Thursday, July 21, 2016

Ubalozi wa Kuwait nchini wakabidhi vitendea kazi kwa Chuo cha Diplomasia


Balozi wa Kuwait nchini, Mhe. Jasem Al-Najem akimkabidhi vitendea kazi zikiwemo Kompyuta kwa Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia (CFR), Dkt. Bernard Achiula. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika Ofisi za Chuo hicho zilizopo eneo la Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi(wa kwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Mhe. Balozi Abdallah Kilima wakiwa pamoja na Mhe. Jasem Al-Najem na Dkt. Achiula ambao waliiwakilisha Wizara katika makabidhiano hayo.
Balozi Mwinyi akiongea na Mhe. Jasem Al-Najem ambapo katika mazungumzo yao walizungumzia namna ya kuimarisha uhusiano uliodumu kwa muada mrefu baina ya mataifa ya Tanzania na Kuwait na alimshukuru kwa kukisaidia chuo hicho ambacho kipo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kumwomba kupanua wigo katika sekta ya Elimu ikiwemo kuwa na program za mafunzo na kubadilishana uzoefu baina y anchi hizi mbili.
Balozi Abdallah Kilima (kushoto) akitoa neno la shukrani kwa Mhe. Balozi Nasem Al-Najem na kueleza namna ambavyo Wizara imejidhatiti katika kuhakikisha inasimamia masuala yote ya Kidiplomasia na ushirikiano.
Mkurugenzi wa Taaluma katika Chuo cha Diplomasia, Dkt. Wetengere Kitojo akifafanua jambo wakati ujumbe huo ulipotembelea Maktaba ya Chuo. Wa pili kutoka kulia ni Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mhe. Balozi Jasem Al-Najem akiendelea kutembelea madarasa na huduma nyingine za wanafunzi katika chuo hicho.
Mhe. Balozi akisalimiana na Wanafunzi wa waliokuwa wakifundishwa somo la lugha ya Kiarabu
Balozi Mwinyi akifafanua jambo kwa Mhe. Al-Najem wakati wakitembelea maeneo ya Chuo hicho.
Dkt.Achiula akikabidhi zawadi ya kinyago kwa Mhe. Balozi Al-Najem ambapo pia alitumia fursa hiyo kumshukuru kwa msaada alioukabidhi kwa Chuo hicho.
Mhe. Balozi Al-Najem akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Diplomasia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.