Thursday, July 21, 2016

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Balozi wa China nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Dkt. Lu Youqing alipofika Wizarani kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na China. Katika mazungumzo yao walijadili namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano hususan katika masuala ya kukuza uchumi  kupitia viwanda na uwekezaji na kuendelea kukamilisha miradi mbalimbali ya pamoja ikiwemo ule wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo Mkoani Pwani.
Sehemu ya Ujumbe kutoka Ubalozi wa China.
Balozi nae akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Katibu Mkuu, Dkt. Mlima
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Christopher Mramba (kushoto) pamoja na Bw. Humphrey Shangarai, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Mlima na Balozi Lu (hawapo pichani)

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.