Tuesday, July 12, 2016

Waziri Mahiga apokea msaada wa madawati 105 kutoka Jumuiya ya Mabohora nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza zoezi la makabidhiano ya madawati kutoka Jumuiya ya Mabohora iliyopo hapa nchini, jumuiya hiyo imechangia jumla ya madawati 105 yenye thamani ya shilingi milioni kumi. Hii ni katika kuiunga  mkono Serikali kwenye zoezi la kuchangia madawati nchi nzima lililo tangazwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Madawati hayo yametengenezwa hapa nchini na Kampuni ya Jambo. Tukio hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora, Mhe. Shehe Zainuddin Adamjee naye akizungumza na waandishi wa habari kwenye makabidhiano ya madawati.
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakisikiliza kwa makini Waziri Mahiga (hayupo pichani)
Sehemu ya wawakilishi wa Jumuiya hiyo wakimsikiliza kwa makini Mhe. Waziri Mahiga
Waziri Mahiga akiwaonyesha waandishi wa habari moja ya dawati kati ya yaliyotolewa na Jumuiya ya Mabohora. Wizara itakabidhi madawati hayo kwa Mamlaka husika  kwa ajili ya kusambazwa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akiwa na Viongozi Wakuu wa Jumuiya ya Mabohora nchini, Mhe. Shekh Tayabali Hamzabhai ( (kushoto) na Shekh Zainuddin Adamjee, Makamu Mwenyekiti (kulia) wakati wa hafla fupi ya kukabidhi madawati.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.