Friday, December 2, 2016

Waziri Mahiga ashiriki maadhimisho ya siku ya Kitaifa ya Umoja wa Falme za Kiarabu

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini Mhe.Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi alipowasili katika ofisi za ubalozi huo kushiriki sherehe ya madhimisho ya miaka 45 ya muungano.Tanzania na UAE zimepiga hatua kubwa za ushirikiano hususan ya kiuchumi ambapo kwa takwimu za Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) hadi Juni, 2015 makampuni 67 ya uwekezaji kutoka UAE yamewekeza hapa nchini katika sekta mbalimbali wenye thamani ya USD 497.12 Millioni na kuajiri Watanzania 9,044. Taifa la Umoja wa Falme za Kiarabu unaundwa na falme saba ambazo ni Abu Dhabi, Dubai, Sharjah, Ras Al Khaimah, Fujairah, Ajman na Umm al-Quwain
                                           
Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Taifa la Umoja wa Falme za Kiarabu Mhe.Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi wakati wa sherehe ya maadhimisho ya miaka 45 ya muungano wa falme hizo

Mhe.Waziri Balozi Dkt.Mahiga akivalishwa skafu maalum

Mhe.Waziri Balozi Dkt. Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mhe.Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi


Wageni waalikwa wakifuatilia jambo

Balozi wa Taifa la Umoja wa Falme za Kiarabu Mhe.Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi akizungumza wakati wa maadhimisho 

Mhe. Waziri Balozi Dkt. Mahiga akitoa hutuba fupi wakati wa maadhimisho ya sherehe hizo


Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdalla Kilima akisalimiana na Mhe. Balozi wakati wa sherehe za maadhimisho
         ------------------------------------------------------------------------------------------------------                                                                  

Tanzania na Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAE) zimepiga hatua kubwa za ushirikiano hususan wa kiuchumi ambapo kwa takwimu za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) hadi Juni, 2015 Makampuni 67 kutoka UAE yamewekeza hapa nchini katika sekta mbalimbali kwa mtaji wa thamani ya Dola za Marekani  milioni  497.12  na kuajiri Watanzania zaidi ya 9,044. 
 
Hayo yalibainishwa jana katika sherehe za kuadhimisha Siku ya Kitaifa ya UAE zilizofanyika jijini Dar Es Salaam ambapo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga alikuwa Mgeni Rasmi. 

Tanzania na UAE  zinatarajiwa kufanya Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) ambao utakuwa chachu ya kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizi mbili hususan ya kiuchumi. 

Akiongea katika hafla hiyo, Mhe. Waziri alilipongeza taifa hilo kwa kuadhimisha siku yake ya Kitaifa ikiwa imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo ya kichumi, kijamii na kisiasa. Mhe.  Waziri alisema kuwa siku hiyo ni inatoa fursa pia ya kutathmini mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Tanzania na UAE.

Kwa upande wake, Balozi wa UAE hapa nchini, Mhe. Abdulla Ibrahim Ghanim Alsuwaidi aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa inayotoa kwa Ubalozi huo ambao unamwezesha kutekeleza majukumu yake kwa wepesi ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano ya nchi hizi mbili. Mhe. Balozi aliahidi kuendeleza ushirikiano huo hususan katika kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda. 

Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) unajumusha falme saba ambazo ni Abu Dhabi, Dubai, Sharjah, Ras Al Khaimah, Fujairah, Ajman na Umm al-Quwain huadhimisha siku yake ya Kitaifa tarehe 02 Disemba ya kila mwaka tokea mwaka 1971.






Thursday, December 1, 2016

Mkutano wa ushirikiano kati ya Afrika na Jamhuri ya Korea kufanyika Addis Ababa

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akizungumza kwenye mkutano na Waandishi wa Habari. Katika mkutano huo Bi. Kasiga aliwaeleza Waandishi wa Habari kuhusu Mkutano wa Nne wa Mawaziri wa nchi za Afrika na Korea utakaofanyika Mjini Addis Ababa, Ethiopia tarehe 06 na 07 Desemba, 2016. Mkutano huo utajadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Afrika na Korea pamoja na maeneo mapya ya mashirikiano.
Afisa Mambo ya Nje, Bi. Bertha Makilagi akifuatilia mkutano kati ya Bi. Kasiga na Waandishi wa Habari. Wengine ni Waandishi wa Habari waliohudhuria mkutano huo.
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakisikiliza na kunukuu kwa makini mkutano uliokua ukiendelea
Mkutano ukiendelea



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mkutano wa Nne wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na Korea ujulikanao kama Korea-Africa Ministerial Forum unaotarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza Barani Afrika, Addis Ababa, Ethiopia tarehe 06 na 07 Desemba, 2016. Mikutano mitatu ya kwanza ilifanyika Seoul, Korea mwaka 2006, 2009 na 2012.

Mkutano huu ambao umeandaliwa na Serikali ya Korea kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika una lenga kukuza ushirikiano pamoja na kuandaa maeneo mapya ya ushirikiano baina ya Korea na mataifa ya Afrika katika miaka mitatu ijayo.

Tanzania ni moja ya nchi nne (4) za Afrika ambazo Korea imezichagua kuanzisha mahusiano ya kimkakati “strategic partnership” yatakayozifanya nchi hizo kupewa kipaumbele katika kupokea misaada na mikopo nafuu kutoka Korea katika kipindi cha miaka mitano ijayo kati ya 2016 hadi 2020.
Katika kipindi hicho, Tanzania itapokea kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 300 ikiwa ni asilimia 17.1 ya msaada utakaotolewa Barani Afrika, hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoongoza Barani Afrika kupokea misaada kutoka Jamhuri ya Korea. Nchi nyingine ni Msumbji, Ethiopia na Angola.
Msaada huo unategemea kufadhili miradi katika sekta za umeme, viwanda na TEHAMA. 

Sanjari na Mkutano huo, ujumbe wa Tanzania utafanya mkutano wa pande mbili na ujumbe wa Serikali ya Korea kuzungumzia masuala ya ushirikiano baina ya nchi zetu mbili. Tanzania itatumia fursa hiyo kuiomba Korea kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi mipya ikiwemo mradi wa Daraja la Selander ambao unatarajiwa kuanza mwaka 2017 na kukamilika 2020.
Aidha, ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano wa Afrika na Korea ni fursa muhimu ya kukuza mahusiano baina ya nchi zetu mbili hususan katika Nyanja ya uchumi. Serikali ya Korea ilitoa ahadi ya kuongeza uwekezaji Barani Afrika hususan katika sekta za nishati, miundombinu na viwanda. 

 Miradi ambayo Tanzania imefaidika tokea kuanzishwa mikutano hii mwaka 2006 ni pamoja na mradi wa kuendeleza kilimo cha Mwani Zanzibar wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 3.6 na Awamu ya Pili ya Mradi wa Huduma ya Uchunguzi wa Afya ya Uzazi Jijini Dar es Salaam wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni nne (4).

Miradi mingine ambayo Jamhuri ya Korea imeshirikiana na inaazimia kushirikiana na Tanzania ni:-
·        Ujenzi wa Mradi wa Daraja la Kikwete kwenye Mto Malagarasi Mkoani Kigoma ambao umekamilika; Ujenzi wa Hospitali ya Kimataifa iliyopo eneo la Mloganzila; Dar es Salaam   na Hospitali ya Mama na Mtoto iliyopo Chanika, Dar es Salaam.

·        Kadhalika, hivi karibuniTanzania imesaini
o   Makubaliano ya kupanua miundombinu ya Majitaka jijini Dar es Salaam; na
o   Makubaliano ya kutekeleza miradi utakaofadhiliwa kwa pamoja na benki ya Maendeleo ya Afrika na Serikali ya Jamhuri ya Korea.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 01 Desemba, 2016.





Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje afungua mkutano wa JPC kati ya Tanzania na Kenya

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Kenya uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo pamoja na mambo mengine utajadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo sekta ya Elimu, Afya na Kilimo.
Balozi wa Kenya hapa nchini, Mhe. Chirau Ali Mwakwere akifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya
Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Bi. Talha Mohammed (kulia) naye akifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa JPC.
Balozi Ben Ogutu, Kiongozi wa Ujumbe wa Kenya akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa JPC kati ya Tanzania na Kenya
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akizungumza wakati wa Mkutano wa JPC kati ya Tanzania na Kenya
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia alikuwa mshereheshaji akizungumza, Bi. Mindi Kasiga
Sehemu ya wajumbe kutoka Kenya wakifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa JPC
Sehemu nyingine ya wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia mkutano

Waziri Mahiga asaini kitabu cha maombolezo ya Rais Mstaafu wa Cuba Fidel Castro

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Cuba nchini Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo alipowasili nyumbani kwa Balozi huyo mapema leo kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais Msataafu wa Cuba Fidel Castrol, Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimfariji Balozi wa Cuba nchini Mhe. Jorge Luis Lopez nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam kabla ya kusaini kitabu cha maombolezo

Mhe. Waziri Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa heshima mbele ya picha ya  Rais wa zamani wa Cuba hayati Fidel Castro alipoenda kusaini kitabu cha maombolezo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisaini kitabu cha maombolezo 

Wednesday, November 30, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Jamhuri ya Korea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo waliyoyafanya Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbalimbali ya kudumisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili (Tanzania na Korea) sambamba na kuzungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea, ikiwemo  mradi wa Hospotali ya Muhimbili, Mloganzila na Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la Sarenda unatarijiwa kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo 

Katika kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga,wengine ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.

Balozi Msechu apokea picha ya kuchora ya Rais Magufuli

Balozi wa Tanzania kwenye Nchi za Nordic na Baltic, Mhe. Dora Msechu amepokea picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kutoka kwa Msanii Mchoraji, Bw. Andrew Dudley Mliga nayeishi nchini Sweden.

 Bw. Mliga amesema kuwa alichukua uamuzi wa kuchora picha ya Mhe. Rais Magufuli baada ya kuhamasishwa  na kazi kubwa anayofanya  Mhe. Rais ya kuweletea maendeleo Watanzania. Ameeleza kuwa yeye ni miongoni mwa wanadiaspora wanaopata faraja kubwa kushuhudia jinsi  mafanikio ya uongozi wa Rais Magufuli  yanavyozidi kung'arisha  jina la Tanzania kwenye ramani ya Dunia.

Balozi Dora Msechu alipokea picha hiyo kwenye moja ya mikutano ya Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Sweden.

Bw. Mliga ni Msanii Mchoraji  anayeishi Sweden ambaye kazi zake zimejikita zaidi kwenye kuitangaza Tanzania kupitia fani ya uchoraji.
  Balozi Dora Msechu akipokea picha ya kuchorwa ya Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli kutoka kwa Msanii Mchoraji, Bw. Andrew Dudley Mliga.       
picha ya kuchorwa ya Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli kutoka kwa Msanii Mchoraji, Bw. Andrew Dudley Mliga.