Saturday, November 28, 2020

UBALOZI WA TANZANIA AFRIKA KUSINI WAPEWA CHANGAMOTO YA KUTEKELEZA DIPLOMASIA YA UCHUMI, SIASA

Na Nelson Kessy, Pretoria

Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini wapewa changamoto ya kuhakikisha kuwa unatekeleza Diplomasia ya Uchumi pamoja na Diplomasia ya Siasa iliyopo ndani ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM (2020-2025).

Changamoto hiyo imetolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge wakati alipotembelea Ubalozi huo jijini Pretoria nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kujionea utendaji kazi wa Ubalozi na mali za Serikali nchini humo. 

Balozi Ibuge ameutaka Ubalozi huo kuhakikisha kuwa unatekeleza diplomasia ya uchumi pamoja na diplomasia ya siasa kwa weledi ili kuleta manufaa ya Taifa.

"Nawapongeza kwa utendaji kazi wenu na nawasihi muendelee kujituma katika kazi (proactive) katika kuwapata wawekezaji na kutengeneza kuwa ni sehemu ya mfumo wa kuleta mabadiliko ambayo Serikali imeyapanga kupitia Ilani ya CCM ya 2020-2025," Amesema Balozi Ibuge.

Balozi Ibuge pia alipongeza utendaji wa Ubalozi huo ambao pamoja na Afrika Kusini unaiwakilisha Tanzania katika Ufalme wa Lesotho, Jamhuri ya Botswana, Jamhuri ya Namibia na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Kadhalika Balozi Ibuge alipokea changamoto mbalimbali zinazoikumba Ubalozi huo na Kuahidi kuzifanyia kazi ili kuongeza tija na ufanisi wa Ubalozi.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali Gaudence Milanzi amemueleza Balozi Ibuge mafaniko mbalimbali ya Ubalozi katika kutekeleza diplomasia ya uchumi na siasa nchini Afrika Kusini.

Moja kati ya mafanikio hayo ni pamoja na kuenezwa kwa lugha ya Kiswahili ambapo Serikali ya Tanzania na ya Afrika Kusini zinatarajia kusaini mkataba wa kutumika lugha ya Kiswahili kama katika shule za Afrika Kusini mwezi wa Machi 2021.

"Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Afrika Kusini tutasaini mkataba wa kutumika kwa lugha ya Kiswahili katika shule za Afrika Kusini mwezi wa Machi 2021," Amesema Balozi Milanzi.

Pamoja na mambo mengine Balozi Milanzi ameahidi kusimamia sera ya Diplomasia ya uchumi pamoja na Diplomasia ya siasa kwa kuhakikisha kuwa ubalozi utaendelea kuwasiliana na wawekezaji mbalimbali wa kuwekeza nchini Tanzania katika sekta za Biashara, Madini na Mawasiliano.


Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akiwatambulisha baadhi ya wafanyakazi kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ibuge wakati alipowasili Ubalozini leo tarehe 27 Novemba 2020


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akisaini kitabu cha wageni katika Ubalozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini leo tarehe 27 Novemba 2020


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akisisitiza jambo kwa watumishi (hawapo pichani) wakati wa mkutano  


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiendesha kikao na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini  


Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akimuonesha baadhi ya mali Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi wakati alipokuwa anakagua mali za Serikali Ubalozini



 

 

 

 

 


Friday, November 27, 2020

SADC-TROIKA, UN KUBORESHA MFUMO WA USALAMA NDANI YA DRC

Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa (UN) zimekubaliana kuboresha mfumo utakao weka ulinzi bora na usalama ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Akithibitisha kuhusu mashirikiano ya mfumo wa kuimarisha ulinzi na usalama nchini DRC, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye amemuwakilisha Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika mkutano huo amesema kuwa kamati ya utatu inayoshughulika na usalama ndani ya jumuiya ya SADC imekutana kwa dharura ili kuweza kuangalia namna ya kukabiliana na matishio ya ugaidi yanayotishia sana hali ya amani na usalama katika nchi zilizopo ukanda wa SADC ikiwemo Msumbiji, Congo DRC na Tanzania.

Mkutano huo wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, nchi zinazochangia Vikosi vya ulinzi na amani vya Umoja wa Mataifa kwenye Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Jamhuri ya Msumbiji  umefanyika leo Tarehe 27, Novemba 2020 mjini Gaborone, Botswana ambapo pamoja na mambo mengine umeangalia masuala mbalimbali yanayohusu amani, ulinzi na Usalama ndani ya SADC.

"Tumeangalia kwa undani mapendekezo mapya ya mfumo wa ulinzi katika enao la DRC ambapo nchi tatu zinazoshiriki katika kuimarisha Ulinzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo nchi tatu zinashiriki kuimarisha ulinzi na usalama nchini DRC (Tanzania, Malawi na Afrika Kusini) kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa zitaendelea kuimarisha masuala ya amani, Ulinzi na usalama Nchini DRC kwa kutumia mfumo mpya utakao weka ulinzi bora na amani nchini DRC," Amesema Mama Samia Suluhu Hassan.

Ameongeza kuwa, kupitia mkutano huo pia limejadiliwa suala la hali halisi ya usalama ndani ya nchi wanachama ndani ya SADC na kuona jinsi ya kutumia usalama wetu kwa ajili ya kujenga uchumi wa ukanda wetu wa kusini mwa Afrika

Kwa upande wake Rais wa Botswana, Dkt. Mokgweetsi Masisi ambae pia alikuwa Mwenyekiti wa Mkutano huo amezipongeza nchi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Visiwa vya Shelisheli kwa kufanya chaguzi ambazo zilikuwa huru, haki na amani na kuzitaka nchi nyingine kuiga mfano huo wa kuwa na demokrisia ya uhuru, amani na haki.

"Matokeo ya chaguzi hizo ni mfano mzuri kwetu sisi kama nchi wanachama wa SADC kujifunza mfano kutoka kwa wenzetu," Amesema Dkt. Masisi.

Dkt. Masisi ameongeza kuwa pamoja kufanya chaguzi huru haki na za amani, kuna mambo ambayo yamekuwa yakijitokeza katika ukanda wa SADC kama vile, Ugaidi, uhalifu wa kimtandao na vikundi vya waasi jambo ambalo limepelekea wakuu wan chi na serikali kukutana hapa (Botswana) na kujadili namna ya kukabiliana na changamoto hizo kwa kuwa changamoto hizi siyo za nchi moja moja bali na kuzitaka nchi zote kuungana na kukabiliana na vikundi hivyo vya kigaidi.

"Mtakumbuka kuwa katika mkutano wetu wa SADC uliofanyika mwezi wa nane mwaka huu tulitoa ripoti iliyoonesha kuwa na baadhi ya ugaidi kwa baadhi ya nchi zetu za SADC, pamoja na ripoti kuonyesha kuwa kuna hali ambayo siyo shwari kwa baadhi ya nchi wananchama, kuna haja ya kuungana pamoja na kuhakikisha kuwa vikundi hivi vya kigaidi vinatokomezwa katika ukanda wetu wa SADC," Amesema Dkt. Masisi.

"Ni jukumu letu sote kuipa ushirikiano Jamhuri ya Kidemocrasia ya Congo hasa upande wa Mashariki mwa DRC na kuhakikisha kuwa amani ya nchi hiyo inalindwa kwa kutokomezwa kwa vikundi vya kigaidi vinavyochangia kutoweka kwa amani nchini humo, na ndiyo maana leo tumekutana hapa ili tuweze kuona na jinsi gani ya kumsaidia mwenzetu DRC," Ameongeza Dkt. Masisi

Pamoja na mambo mengine, Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama  inawajibika kukuza amani na usalama katika eneo la SADC na pia ina wajibu wa kuongoza na kuzipatia nchi Wanachama mwongozo kuhusu mambo ambayo yanatishia amani, ulinzi na usalama.

Ni mara ya kwanza kwa Wakuu wan chi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC - TROIKA) kukutana ana kwa ana tangu ulipotokea ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu (Covid-19).

Mkutano huo ulihudhuriwa na, Rais wa Botswana Mhe. Dkt. Mokgweetsi Masisi, Rais wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa, Rais wa Malawi Mhe. Lazarus Chikwera, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mhe. Felix Tshisekedi, Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Msumbiji Bw. Jaime Neto aliyemuwakilisha Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati wa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, nchi zinazochangia Vikosi vya ulinzi na amani vya Umoja wa Mataifa kwenye Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Jamhuri ya Msumbiji  uliofanyika leo Tarehe 27, Novemba 2020, mjini Gaborone Botswana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati wa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, nchi zinazochangia Vikosi vya ulinzi na amani vya Umoja wa Mataifa kwenye Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Jamhuri ya Msumbiji  uliofanyika leo Tarehe 27, Novemba 2020, mjini Gaborone Botswana

Wakuu wa Nchi na Serikali wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, nchi zinazochangia Vikosi vya ulinzi na amani vya Umoja wa Mataifa kwenye Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Jamhuri ya Msumbiji  uliofanyika leo Tarehe 27, Novemba 2020, mjini Gaborone Botswana





Thursday, November 26, 2020

MAWAZIRI SADC - TROIKA WAKUTANA KWA DHARURA BOTSWANA

 Baraza la Mawaziri wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama wakutana katika mkutano wa dharura na kujadili masuala ya siasa, ulinzi na usalama.

Mkutano huo umefanyika leo mjini Gaborone, Botswana ambapo ulitanguliwa na mkutano wa Makatibu Wakuu wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ulioanza asubuhi na kumalizika mchana.

Kupitia mkutano huo, mawaziri wameweza kujadili masuala ya hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda ya SADC na kupendekeza njia mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kwenye siasa, ulinzi na usalama ndani ya ukanda wa SADC.

Pamoja na mambo mengine, Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama  inawajibika kukuza amani na usalama katika eneo la SADC na pia ina wajibu wa kuongoza na kuzipatia nchi Wanachama mwongozo kuhusu mambo ambayo yanatishia amani, ulinzi na usalama.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (mwenye tai nyekundu) akifuatilia mkutano wa dharura wa baraza la Mawaziri wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama uliofanyika Mjini Gaborone. Kulia mwa Waziri ni Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Faraji Mnyepe akifuatiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge

Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ukiwa ukiimba wimbo wa SADC kabla ya kuanza kwa mkutano wa dharura wa baraza la Mawaziri


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Botswana Dkt. Lemogang Kwape akifungua mkutano wa Dharura wa baraza la mawaziri, kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stegomena Taxi

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stegomena Taxi mara baada ya kumaliza mkutano wao     


MAKATIBU WAKUU SADC - TROIKA WAKUTANA KUJADILI SIASA NA USALAMA

Makatibu Wakuu wa SADC -TROIKA wamekutana na kujadiliana Mambo mbalimbali yakiwemo masuala ya hali ya Siasa, Ulinzi na Usalama ndani ya SADC mjini Gaborone, Botswana.

Awali, Mkutano wa Makatibu Wakuu ulifunguliwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Botswana, Bw. Gaeimelwe Goitsemang ambae pia alikuwa Mwenyekiti wa Mkutano huo.

Ni mara ya kwanza kwa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ( SADC) kukutana ana kwa ana tangu ulipotokea ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu (Covid-19).

Kwa upande wa Makatibu wakuu waliohudhuria katika Mkutano huo kutoka Tanzania ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe.

Mkutano wa Makatibu Wakuu utafuatiwa na Mkutano wa Dharua wa Baraza la Mawaziri wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano katika Siasa, Ulinzi na Usalama baadae mjini Gaborone.


Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ukifuatilia Mkutano wa Makatibu Wakuu wa SADC -TROIKA uliofanyika mjini Gaborone, Botswana


Mkutano wa Makatibu Wakuu wa SADC -TROIKA ukiendelea

Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ngazi ya Makatibu Wakuu ukifuatilia mkutano  

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akiwasilisha mada katika Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Asasi ya SADC ya ushirikiano katika siasa, ulinzi na Usalama unaondelea Mjini Gaborone, Botswana



 

 

VACANCY ANNOUNCEMENT



VACANCY ANNOUNCEMENT

Applications are hereby invited from qualified and experienced Tanzanians for the following vacant post advertised by the Southern African Development Community (SADC) Secretariat:- 

1.0 Vacant Position 

1. Deputy Executive Secretary Regional Integration (25 years of professional experience of which at least 10 years in a top leadership position in a public/private organization, regional or international institution)

2.0 Eligibility

All qualified Tanzanians aged not more than 50 years old are eligible to apply. 

3.0 Closing Date for the Submission of Applications:

All applications must be submitted not later than 10th December, 2020. Applications should be accompanied by the following:

a) A cover letter describing the applicant’s academic qualifications, experience and competencies relevant to the position;

b) A five (5) page current Curriculum Vitae;

c) Certified copies of the applicant’s Degree(s), Diploma(s) and Certificate(s); 

4.0 Submission of Applications

Two hard copies of applications must be submitted to the President’s Office Public Service Management and Good Governance - Dodoma Office Room No. 217B and 221B by hand or mailed to the following address:


Permanent Secretary,

President’s Office,

Public Service Management and Good Governance,

College of Business Studies and Law,

Government City Mtumba,

P.O. BOX 670, 

DODOMA. Attention: Human Resources Development Division.


5.0 Gender Mainstreaming

SADC is an equal opportunity employer and encourage applications from female candidates.


NB:

- Only applicants who meet the requirements of the SADC Secretariat and being considered for interview will be contacted. 

- Shortlisted applicants’ will be required to present original copies of their academic qualifications during the interview.



Wednesday, November 25, 2020

Mama Samia kumwakilisha JPM Mkutano wa SADC Organ Troika

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi


Na Nelson Kessy, Gaborone-Botswana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kumwakilisha Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwenye Mkutano wa dharura wa pamoja baina ya SADC Organ Troika (Botswana, Malawi na Zimbabwe), na nchi zinazochangia Vikosi vya ulinzi na amani vya Umoja wa Mataifa, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwenye Kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC utakaofanyika tarehe 28 Novemba 2020, mjini Gaborone, Botswana.

Akithibitisha kuhusu ushiriki wa Tanzania katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema kuwa ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo utaongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye atakuwa anamwakilisha Mhe. Rais.

Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, mkutano huu utatanguliwa na mkutano wa Maafisa Waandamizi/Makatibu Wakuu wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama na kufuatiwa na mkutano wa Dharura wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama tarehe 26 Novemba 2020.

"Pamoja na Mambo mengine, mkutano huo utajadili hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda ya SADC na kuweza kuona changamoto mbalimbali zilizojitokeza na kupata majibu ya kutatua changamoto hizo," Amesema Prof. Kabudi

Makamu wa Rais ataambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi Dkt. Faraji Mnyepe pamoja na Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda na Mratibu Kitaifa wa Masuala ya SADC, Bibi Agnes Kayola.

ASASI ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama (Troika) ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) inawajibika kukuza amani na usalama katika eneo la SADC na pia ina wajibu wa kuongoza na kuzipatia nchi Wanachama mwongozo kuhusu mambo ambayo yanatishia amani, ulinzi na usalama.


FURSA YA AJIRA JUMUIYA YA MADOLA


 

Tuesday, November 24, 2020

TANZANIA YAITHIBITISHIA JUMUIYA YA KIMTAIFA KUENDELEA KULINDA AMANI AFRIKA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeihibitishia jumuiya ya kimataifa kuwa itaendelea kutoa vikosi vya kulinda amani na ulinzi katika nchi za bara la Afrika.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipokuwa katika mkutano wa kunzindua kikosi kazi cha kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa juu ya wanawake, amani na usalama jijini Dar es Salaam.

Prof. Kabudi amesema kuwa serikali ya Tanzania ipo tayari kufanya kazi kwa kushirikiana na Shirika la Mwalimu Nyerere na Shirika la Umoja wa Mataifa pamoja na mashirika mengine duniani katika kuhakikisha kuwa amani ulinzi na usalama vinapatikana.

"Tanzania imekuwa ni nchi mojawapo inayotoa askari wanaokwenda kulinda amani katika mataifa mbalimbali katika bara la Afrika ambapo baadhi yake ni Sudani, Congo DRC, Lebanon na Afrika ya Kati……… kwa hiyo lengo la mpango kazi huu ni kuwezasha Serikali ya Tanzania kuboresha ushiriki wa askari wa kike katika masuala ya ulinzi na amani," Amesema Prof. kabudi

Aidha, Prof. Kabudi ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kutoa askari wa kulinda amani katika mataifa mbalimbali barani afrika kwani suala la amani katika jamii ni jambo muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa lolote lile Duniani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, amesema kuwa Taasisi anayoiongoza iko tayari kufanya kazi kwa karibu na jumuiya ya kimataifa na washirika wote wa maendeleo katika kuhakikisha kuwa amani na utu wa mwanamke unalindwa na kuheshimiwa katika jamii.

Pamoja na mambo mengine, mkutano huo pia ulihudhuriwa na mabalozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, akiwemo Balozi wa Norway, Mhe. Elisabeth Jacobsen, Balozi wa Nchi za Falme za Kiarabu, mhe. Khalifa Abdulrahman Mohammed Ali-Marzouki, Balozi wa Canada Mhe. Pamela O'Donnell pamoja Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan MiliÅ¡ić.  

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku akiongea wakati wa Mkutano wa kunzindua kikosi kazi cha kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa juu ya wanawake, amani na usalama jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akihutubia hadhara iliyohudhuria mkutano wa uzinduzi wa kikosi kazi cha kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa juu ya wanawake, amani na usalama jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki

 

Sunday, November 22, 2020

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA SADC WA TROIKA MBILI NA WASHIRIKA WA MAENDELEO




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Tanzania yashiriki Mkutano wa SADC wa Troika Mbili na Washirika wa Maendeleo 


Dodoma, 21 Novemba 2020
Tanzania imeshiriki Mkutano wa SADC wa Troika Mbili (SADC Double Troika na Washirika wa Maendeleo (International Cooperating Partiners- ICPs) uliofanyika tarehe 19 na 20 Novemba, 2020 kwa njia ya mtandao. 

Lengo la Mkutano huo lilikuwa ni kujadili na kutoa maamuzi kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya SADC na Washirikia wa Maendeleo. Yafuatayo ni baadhi ya masuala yaliyojadiliwa na kutolewa maamuzi kwenye mkutano huo: -

1. Mkutano ulipokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa maazimio                                                                                                      ya mkutano uliotangulia wa SADC/ICPs uliofanyika mwezi Disemba, 2019. Aidha, mkutano huo ulijiridhisha kwa hatua iliyofikiwa katika kutekeleza ajenda ya ushirikiano wa SADC/ICPs. Miongoni mwa maeneo yaliyotolewa taarifa ya mafanikio ni pamoja na kukutana kwa Kamati Maalum za Wataalam ambazo zimeendelea kudumisha ushirikiano baina ya pande hizo mbili;

2. Mkutano ulipokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Mpango Mkakati Elekezi wa Maendeleo wa Kanda (Regional Indicative Strategic Development Plan (RISDP 2020-2030) na Dira ya SADC (yaani SADC Vision-2050); katika ajenda hii SADC iliwasilisha ombi la ufadhili wa utekelezaji wa mpango huo. Aidha, baada ya majadiliano, upande wa ICPs ulikubali kutoa ufadhili kwa ajili ya utekelezaji.

3. Mkutano ulijadili athari za mlipuko wa COVID-19 katika SADC na hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kukabiliana na athari hasi za ugonjwa huo; Katika ajenda hii Nchi wanachama ziliomba ICPs kufadhili maboresho ya viwanda vya ndani ambavyo vimejikita katika kuzalisha vifaa tiba, vifaa kinga na madawa na upande wa ICPs ulikubali kuendelea kuifadhili SADC. 

4. Mkutano uliijadili taarifa ya maboresho ya ukanda wa kijani (Green Recovery) na mkakati wa SADC wa uchumi wa kijani (SADC Green Economy Strategy). Ushirikiano huu kwa vitendo unahusu hifadhi ya mazingira na uchumi endelevu kama nyenzo ya kufikia maendeleo endelevu katika ukanda wa SADC. Pamoja na mambo mengine masuala yatakayotekelezwa katika eneo hili yanalenga katika kukabiliana na changamoto za uharibifu wa Mazingira katika SADC. Changamoto hizo ni pamoja na uchomaji wa misitu, mabadiliko ya tabianchi, mmomonyoko wa udongo, kuenea kwa hali ya jangwa na ukame, upotevu wa bioanuai (loss of biodiversity), ukosefu wa ajira, changamoto za kiuchumi na kibiashara zitokanazo na bei ya nishati. mashirikiano katika eneo hili yatajikita katika kugeuza changamoto husika kuwa fursa; na 

5. Pamoja na hayo, kikao kilipitia na kujiridhisha utekelezaji wa masuala mtambuka ya ushirikiano kupitia Kamati za Wataalam za Kipaumbele (Thematic Groups) zinazoratibu masuala ya ushirikiano wa ulinzi na usalama, usafirishaji, nishati, maji, udhibiti wa athari za majanga, afya, kilimo, TEHAMA na mabadiliko ya tabia nchi.

Itakumbukwa kuwa, Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC ulifanyika mwezi Agosti, 2019 Dar es salaam, Tanzania, pamoja na mambo mengine, Mkutano huo ulielekeza itengwe siku maalum ya tarehe 25 Oktoba, 2020 kwa kila mwaka ili kupaza sauti hadi hapo vikwazo kandamizi vya kiuchumi vilivyowekwa nchini Zimbambwe na nchi za Magharibi viweze kuondolewa. Sambamba na hilo, mkutano huo uliagiza Nchi wanachama kupaza sauti katika majukwaa mbalimbali, Kwa namna ya kipekee, Tanzania ilitumia fursa ya mkutano huo, kupaza sauti kwa ajili ya kuondolewa kwa vikwazo kandamizi vya kiuchumi vilivyowekwa dhidi Jamhuri ya Zimbabwe.

Mkutano huo, uliongozwa na Jamhuri ya Msumbiji ambaye ni Mwenyekiti wa sasa wa SADC kwa kushirikiana na mwenyekiti mwenza kwa upande wa ICPs. Katika Mkutano huo, Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Bi. Agnes R. Kayola, Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mkutano kama huo, utaitishwa tena mwaka 2021 kulingana na ratiba na hadidu za rejea za kuendesha vikao vya namna hiyo. 


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali



Saturday, November 21, 2020

PROF. KABUDI: TUTASHIRIKIANA NA TAIFA LOLOTE LINALOIHESHIMU TANZANIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema Tanzania itashirikiana na nchi yoyote duniani ambayo inatambua na kuheshimu Uhuru wa nchi na utu wa watu wake. 


Prof. Kabudi ametoa kauli hiyo jijini Dodoma alipozungumza na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na taasisi zake tangu alipoteuliwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuwa Waziri wa Mambo ya Nje. 

"Tutafanya kazi na nchi zote ambazo zinatuheshimu, zinatutambua kama Taifa huru, kutuheshimu sisi kama binadamu wa mataifa mengine, hatutakubali kudharauliwa, kutokuheshimiwa utu wetu na kudharauliwa kwa sababu ya misaada au pesa’, amesema Prof. Kabudi 

Ameongeza kuwa Tanzania itasikiliza taifa lolote duniani na kujadiliana nalo kwa heshima kwani mapungufu hayapo upande mmoja tu. 

"Tuko tayari kuwasikiliza na kujadiliana nao kwa heshima na kama wanadhani kuna kitu kimepungua kwetu na sisi tunadhani kimepungua kwao," amesema Prof. Kabudi. 

Amesema Tanzania haiwezi kumruhusu mtu yeyote atumie misaada ya fedha kuondoa uhuru wetu na kutokuthamini utu wetu. 

Amesema Tanzania haiwezi kujitenga kama kisiwa na itaendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za kidunia kama vile kulinda amani, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kutunza mazingira. 

"Hatutajitenga katika dunia hii, tutaendelea kujumuika katika kazi mbalimbali kama vile ulinzi wa amani, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuhifadhi mazingira,’ alisema na kuongeza kuwa tumekuwa bandari ya amani kwa wakimbizi sio tu kutoka Afrika bali duniani kote na tutaendelea kuwa hivyo," Ameongeza Prof. Kabudi. 

Prof. kabudi pia amewataka watumishi wa Wizara kusoma kitabu cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alichowaandikia watumishi wa wizara hiyo mwaka 1969 cha Usipayuke toa hoja ‘Don’t shout argue’ ili kutoa takwimu sahihi kwa wakati. 

Amesema jukumu la kuieleza dunia kuhusu takwimu za vitu mbalimbali ni la watumishi wa Mambo ya Nje na hawana budi kuhakikisha wanaliekeleza hilo kwa ufasaha. 

Mbali na kitabu hicho, Prof. Kabudi amewakabidhi wakurugenzi wa Idara mbalimbali Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hotuba za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wakati anafungu Bunge la 11 na hotuba ya ufunguzi wa Bunge la 12 na kuwataka kusimamia na kutekeleza maagizo yote yaliyopo kwenye hotuba hizo pamoja na maelekezo ya Ilani ya CCM. 

Awali akimkaribisha Waziri kuzungumza na watumishi, Katibu Mkuu Wizara Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wibert Ibuge aliwapongeza watumishi utendaji mzuri wa kazi na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii na uadilifu.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) alipokuwa anawasili kwenye kikao cha wafanyakazi jijini Dodoma


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiongea na watumishi (hawapo pichani) kwenye mkutano wa Waziri Prof. Kabudi na Watumishi wa Wizara ulifanyika Jijini Dodoma


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge Ilani ya CCM na nyaraka nyingine za utendaji  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)akimkabidhi nyaraka Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora Balozi, Anisa Mbega


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)akimkabidhi nyaraka Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Bibi. Caroline Chipeta  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)akiongea na Watumishi wa wizara  katika mkutano uliofanyika jijini Dodoma



Friday, November 20, 2020

TANZANIA YAAHIDI KUENDELEA KUISAIDIA CONGO KULINDA AMANI UKANDA WA MAZIWA MAKUU

 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeahidi kuendelea kuisaidia Congo kulinda amani na kuhakikisha changamoto za  ulinzi na usalama zinazoikabili nchi hiyo zinatatuliwa ili kuimarisha hali ya amani katika Ukanda wa Maziwa Makuu.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) alipokuwa akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika Mkutano wa Nane wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) uliofanyika kwa njia ya video (Video Conference).

"Tanzania tutaendelea kusaidia juhudi za kuimarisha ulinzi na usalama katika eneo la mashariki mwa Congo - DRC kwani kukosekana kwa utulivu wa kisiasa na kiusalama kwa nchi hiyo kunahatarisha usalama wa eneo lote la Jumuiya nzima ya ICGLR nayo itakuwa salama," amesema Prof. Kabudi.

Ameongeza kuwa Congo Brazaville ilikuwa ikikabiliwa na uasi kutoka kundi la Ninja lililokuwa  likiisumbua Serikali  kwa miaka mingi hata hivyo hadi kufikia katikati ya mwaka 2019 uasi ulitulia kufuatia mazungumzo ya kusitisha  mapigano kati ya kundi hilo na Serikali.

Amesema Congo-Kinshasa na Congo-Brazaville ni muhimu katika eneo la maziwa makuu kutokana na kuwepo kwa asilimia kubwa ya rasilimali za misitu, maji na madini ambavyo vinahitajika sana duniani na kuongeza kuwa umuhimu zaidi unahitajika kutokana na ukweli kuwa kuna haja kubwa ya kutunza mazingira, kuzalisha nishati na kukuza uchumi wa dunia.

"Nchi hizi mbili za DRC na Congo Brazaville ni nchi muhimu sana katika eneo la Maziwa Makuu kutokana na kuwepo kwa asilimia kubwa ya rasilimali, baadhi ya rasilimali hizo kama misitu, maji na madini zinahitajika sana duniani kwa sasa kutokana na umuhimu wake, umuhimu ambao unatokana na haja ya kutunza na  kulinda mazingira, uzalishaji wa nishati na kukuza uchumi wa dunia," alisema n kuongeza kuwa Kukosekana kwa utulivu wa kisiasa na kiusalama katika nchi hizi kunahatarisha usalama wa eneo lote la Maziwa Makuu ikiwemo na usalama wa dunia kutokana na uwezekano wa baadhi ya mataifa makubwa kugombea rasilimali hizo", alisisitiza Prof. Kabudi.

Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya ICGLR umepokea na kujadili taarifa mbalimbali kuhusu Jumuiya hiyo , mbali na hali ya kisiasa na kiusalama katika Ukanda huo umeangalia pia suala la michango ya wanachama katika bajeti ya Sekretariat na Mfuko Maalum wa maendeleo, taarifa ya mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya, taarifa ya mkutano wa Mawaziri wa Ulinzi  kuhusu hali ya usalama wa Ukanda wa Maziwa Makuu na taarifa ya mkutano wa Mawaziri wa Afya.

Nchi wanachama wa ukanda wa maziwa makuu ni pamoja na Angola, Burundi, Jamhuri ya Kati, Demokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kongo, Kenya, Rwanda, Sudan, Sudani Kusini, Tanzania, Uganda na Zambia.

Oktoba 2019, Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ulifanyika nchini Congo Brazzaville.

Katika tukio jingine, Prof. Kabudi amekutana na kumuaga Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru ambapo pamoja na mambo mengine amemshukuru Bw. Mubiru kwa mema aliyoyafanya hapa nchini hasa katika kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua kimaendeleo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akifuatilia Mkutano wa Nane wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) uliofanyika kwa njia ya video (Video Conference) jijini Dodoma

Rais wa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi akizungumza katika mkutano wa Nane wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) 


Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Bw. António Guterres akizungumza katika mkutano wa Nane wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR)


Rais wa Jamhuri wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame akizungumza katika mkutano wa Nane wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR)