Wednesday, March 24, 2021

VIONGOZI WAKUU WA NCHI NA SERIKALI DUNIANI WASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA JPM

 

Rais wa Burundi Mhe. Ăˆvariste Ndayishimiye akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Tanzania nchini Burundi kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle-Work Zewde akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli

Naibu Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Ulinzi wa Serikali ya Oman, Mtukufu Sayyid Shihab bin Tarik bin Taimur Al-Said, akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 

 


WAZIRI MKUU AONGOZA WAKAZI WA MWANZA KUMUAGA JPM

Na Mwandishi wetu, Mwanza

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameongoza maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na mikoa jirani kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Waombolezaji walianza kuingia uwanjani leo alfajiri na wengine wakiwa wamejipanga barabarani kuulaki msafara wa mwili wa Hayati Magufuli ukitokea Zanzibar.

Mhe. Majaliwa aliongozana na mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na viongozi wa taasisi za umma na binafsi katika hafla ya kutoa heshima za mwisho kwa kwa hayati Dkt. Magufuli anayetarajiwa kuzikwa nyumbani kwake Chato Machi 26, 2021.

Wengine waliohudhuria ni pamoja na wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama wakiongozwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa salamu za pole kwa wananchi wa Mwanza katika hafla kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli


Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipowasili katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza katika hafla kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli


Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akitoa heshima za mwisho katika uwanja wa CCM Kirumba wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli


Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa CCM Kirumba    

Wananchi wa Jiji la Mwanza wakiwa barabarani kushuhudia msafara uliobeba mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli 






 

Monday, March 22, 2021

HABARI PICHA MWILI WA HAYATI DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI UKIAGWA JIJINI DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Lazarius Chakwera akipokelewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge wakati alipowasili katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta akisaini kitabu cha maombolezo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli


Rais wa Muungano wa Visiwa vya Comoro Mhe. Azali Assoumani akisaini kitabu cha maombolezo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli




Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa akisaini kitabu cha maombolezo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma baada ya kuwasili kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia Taifa wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli yaliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa akitoa salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Mhe. Felix Tshisekedi akitoa salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Mjane wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akitoa heshima za mwisho kwa mume wake hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Lungu akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) Dkt. Stergomena Tax akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Baadhi ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma


Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akitoa heshima za mwisho kwa Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli wakati wa mazishi ya kitaifa katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma 


Sehemu ya wananchi waliojitokeza katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma wakati wa mazishi ya kitaifa ya Rais wa Tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli  



Sunday, March 21, 2021

DODOMA WAENDELEA KUMLILIA MHE. DKT. MAGUFULI


Viongozi wa Serikali, Kitaifa na Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya jijini Dodoma wameendelea kumlilia aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 Machi, 2021 jijini Dar es Salaam. 

Wananchi hao wamejitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nyerere Square jijini humo kusaini kitabu cha maombolezo. Wananchi hao pia wameelezea hisia zao jinsi walivyokea msiba huo na walivyomfahamu Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. 

Akiandika katika kitabu cha Maombolezo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge ameelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo na kusema kuwa atamkumbuka daima Hayati Magufuli kwa jinsi alivyojitoa kuwatumikia wananchi wa Tanzania. " Kwa uchungu na masikitiko makubwa sana sababu Watanzania tumempoteza kiongozi na mpenda maendeleo aliyejipanga kuwaletea maendeleo ya kweli Watanzania," ameandika .

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Ajira na Mbunge wa Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ameelezea hisia zake kwa kuandika "Tunakushukuru na kumshukuru kwa zawadi ya uhai wako uliyoitoa kwa Watanzania kizalendo kuwapigania, Mungu kazi sake haina makosa. Taifa limetikisika tutakuenzi kwa mema mengi, uongozi bora, uzalendo, maendeleo, upendo, amani na taifa".

 
Kwa upande wake Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia alijitokeza katika viwanja vya Nyerere Square kusaini kitabu cha maombolezo ameelezea hisia zake akisema “Hayati Dkt. Magufuli ametutoka katika kipindi ambacho tulikuhitaji sana. Watanzania tunakupenda na tutaendelea kukuoenda kwa matendo na mambo mema uliyotufanyia na kutuachia kama Taifa”. Aliendelea kueleza kuwa Afrika imepoteza shujaa na mtetezi wa Bara.

Wakati huo huo Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Mhe. Dormohamed Issa Rahmat amesema “Kwa majonzi, masikitiko na maumivu makubwa tuliyonayo Watanzania kwa kuondokewa na mzalendo namba moja, Jemedari wa Maendeleo na shujaa wa kupambania maskini na wanyonge. Sina cha kusema zaidi ya kumshukuru Mungu na kumuomba ialaze Roho ya Marehemu Mahala pema Peponi”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw. Mohamed Ramadhani ameeleza “Mheshimiwa Rais ulikuwa kiigizo chema kwetu, umeweza kutufumbua Watanzania kuwa hakuna kinachoshindikana panapo dhamira ya dhati tukiamua kufanya masuala ya msingi katika kutatua changamoto zinazoikabili nchi yetu, tutakuenzi kwa kuendeleza yale uliyoyanzisha huku tukitambua na kuzingatia kauli yako ya vita ya kiuchumi hakuna Mataifa yasiyo na nia njema yatakayo tupenda. Pumzika kwa amani Jemadari Wetu Mungu akujalie Pepo”. 

Mwili Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli umewasili jijini Dodoma majira ya saa 10 jioni kutokea Dar es Salaam na kupokelewa na Wananchi wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Dkt, Benelith Mahenge na Viongozi weinigen wa Serikali.

Mwili wa Hayati Dkt. Magufuli umepitishwa katika Mitaa mbalimbali ya Jiji la Dodoma na kuelekea Ikulu Chamwino. Tarehe 22 Machi, 2021 ataagwa rasmi na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye kueleekea katika uwanja wa Jamhuri. Miongoni mwa shughuli zitakazofanyika Uwanjani hapo ni pamoja na gwaride la mazishi kutoka Jeshi la Wananchi la Tanzania, dua na sala, salamu za maombolezo na kutoa heshima za mwisho.

Jumanne Machi 23, 2021 saa 12 asubuhi mwili wa Hayati Dkt. Magufuli utatolewa katika hospitali ya Banjamin Mkapa na kusafirishwa kuelekea Zanzibar.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Patrobas Katambi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

Mke wa Rais wa Awamu ya Nne na Mbunge wa Jimbo la Mchinga mkoani Lindi Mhe. Salma Kikwete akitia saini katika kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

Sheikh wa Mkoa wa Dodoma Mustafa Rajabu akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

Wakazi wa jijini Dodoma wakiwa katika Viwanja vya Nyerere Square jijini humo kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

Mtoto huyu alikuwa miongoni mwa wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

Mwanahabari kutoka Television ya Serbia akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 17, Machi 2021.

























Saturday, March 20, 2021

MARAIS WASTAAFU, VIONGOZI WAANDAMIZI WA SERIKALI NA MABALOZI WAMLILIA MAGUFULI

Na mwandishi wetu

Marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi waandamizi wa Serikali na mabalozi waonaziwakilisha nchi zao hapa Nchini wamewataka watanzania kuendelea kudumisha uzalendo, fikra na maono aliyokuwa nayo Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ili kuiwezesha Tanzania kukua kimaendeleo

Akizungumza mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete amesema kifo cha Hayati Magufuli hakikutarajiwa hasa wakati huu ambapo taifa lilimuhitaji na kuwasihi watanzania kudumisha mema aliyoyaasisi kwa maslahi ya taifa.

“Kwa kweli kifo chake hakikutarajiwa, tulitegemea kwa kweli aendelee kuliongoza taifa kwani katika mhula wake wa kwanza aliliongoza taifa vizuri sana…….naamini kuwa yale ambayo hayakukamilika, Rais wa Jamhuri ya Tanzania mhe. Samia Suluhu Hassan atayaendeleza kikamilifu,” Amesema Dkt. Kikwete na kuwasihi watanzania kuendelea kudumisha uzalendo, fikra na maono aliyokuwa nayo Hayati Dkt. Magufuli.

Rais wa Awamu ya Pili, Mhe. Alhaji Ali Hassan Mwinyi nae amefika katika viwanja vya Karimjee na kusaini kitabu cha maombolezo akifuatiwa na Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mohamed Gahib Bilali, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma na pamoja na Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai nae pia amefika na kusaini kitabu hicho akifuatiwa na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar mhe. Zubeir Ali Maulid ambaye amesema kuwa Hayati Magufuli katika kipindi kifupi cha uongozi wake amefanya mambo mengi yatakayosalia kuwa historia katika taifa la Tanzania.

“Msiba huu ni wetu sote watanzania na umetugusa sana kwani  hayati Magufuli ameyafanya mengi katika mhula wake wa kwanza ambapo mengi hayo tumekuwa tukinufaika nayo sisi watanzania…..kwa sasa tushikamane kudumisha umoja wetu ili kuweza kusonga mbele kimaendeleo,” Amesema Mhe. Maulid

Aidha, mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini nao wameungana na watanzania kuomboleza kifo cha Hayati Dkt. Magufuli kwa kusaini kitabu cha maombolezo ambapo baadhi yao wamemuelezea kuwa katika uhai wake Hayati Magufuli alitamani kuiona Tanzania inayojitegemea kiuchumi na watu wake kuondokana na umasikini.

Naibu Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Mhe. Prefere Ndayishimiye amesema kuwa msiba wa Hayati Magufuli umewagusa sana kwani alikuwa kiongozi aliyependwa na kujulikana na bara lote la Afrika.

“Amefanya maendeleo makubwa ambapo naamini kuwa vizazi vijavyo vitayaona na kuendeleza pale alipoishia Dkt. Magufuli,” Amesema Naibu Balozi

Kadhalika, mbali na viongozi wastaafu pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali wananchi wa kada mbalimbali wamejitokeza kwa wingi kusaini kitabu cha maombolezo na kumuelezea hayati Magufuli kuwa alikuwa kiongozi aliyeweka maslahi ya nchi mbele kwa manufaa ya watanzania.

Rais wa Mstaafu wa awamu ya pili Mhe. Alhaj Ali Hassan Mwinyi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021  


Rais wa Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 


Makamu wa Rais, Mstaafu Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Joseph Magufuli  


Spika wa Baraza la Wawakilishi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar mhe. Zubeir Ali Maulid akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli   


Balozi wa Oman nchini Tanzania, Mhe. Ali Abdulla – Al Mahrouq akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Somalia nchini Tanzania, Mhe. Mohamed Hassan Abdi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Misri nchini Tanzania, Mhe. Mohamed Gaber Abulwafa akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Mhe. Jaafer Nasir Abdalla akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli   


Naibu Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberte Cocconi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli



Friday, March 19, 2021

RAIS SAMIA AONGOZA VIONGOZI, MABALOZI MBALIMBALI KUASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaongoza viongozi waandamizi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akiwemo Rais Dkt Hussein Ali Mwinyi kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli huku baadhi ya mabalozi wakibubujikwa na machozi.

Rais Samia Suluhu Hassan amesaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Kamrijee Dar es Salaam mchana wa leo na kufuatiiwa na baadhi ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania kufuatia kifo cha aliyekuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021 katika hospitali ya Mzena kwa maradhi ya moyo.

Pia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Hussein Ally Mwinyi nae pia amesaini kitabu cha maombolezo akifuatiwa na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe Othaman Masoud

Baadhi ya Mabalozi wanaoziwakilisha Nchi zao hapa Nchini walishindwa kujizuia na kutokwa na machozi kumlilia Hayati Dkt. Magufuli na kumuelezea kuwa alikuwa kiongozi jasiri na mzalendo si kwa manufaa ya Tanzania pekee bali Afrika kwa ujumla ambapo Balozi wa Jamaica hapa nchini Mhe. Velisa Delfosse amemuelezea Hayati Dkt Magufuli kama mwanampinduzi na mzalendo halisi wa Afrika wa wakati huu

“Rais Magufuli alikuwa mwanampinduzi na mzalendo halisi wa Afrika wa wakati huu, kwa kweli tumeguswa sana na msiba wake hakika pengo lake halitazibika, tunamuombea kwa Mungu apumzike salama,” Amesema Balozi Delfosse

Nae Balozi wa China hapa Nchini Mhe. Wang Ke mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo amemuelezea Hayati Magufuli kama kiongozi mwenye maono na mzalendo mwaminifu kwa Afrika,na kwamba atakumbukwa na Watanzania kwa jitihada zake kubwa za kuleta mabadiliko chanya  ili kuinua hali ya maisha hususani wale wa kipato cha chini.

Kwa upande wake Balozi wa Sudani ya Kusini Mhe. William Ruben amewasihi viongozi wa Afrika na Watanzania kwa ujumla kufuata nyayo za Hayati Dkt Magufuli kwa kuwa alikuwa alama halisi ya Afrika na alitufundisha wengi wetu kuamini kuwa Afrika imebarikiwa na ni tajiri kinyume na tulivyoamini kuwa tunahitaji msaada kutoka kwa mataifa ya nje ya bara la Afrika 

“Naomba kuwasihi viongozi wa Afrika na Watanzania kwa ujumla kufuata nyayo za Hayati Dkt Magufuli kwa kuwa alikuwa alama halisi ya Afrika na alitufundisha wengi wetu kuamini kuwa Afrika imebarikiwa na ni tajiri kinyume na tulivyoamini kuwa tunahitaji msaada kutoka kwa mataifa ya nje ya bara la Afrika,” Amesema Balozi Ruben

Mabalozi wengine waliofika katika viwanja vya Karimjee na kusaini kitabu cha maombolezo ni pamoja na Balozi wa Morocco Mhe. Abdililah Benryane, Balozi wa Ethiopia Mhe Yonas Sanbe, Balozi wa Qatar Mhe Abdulla Jassim Al Madadadi, Balozi wa Japan Mhe Shinichi Goto Balozi wa Palestina Mhe Derar Ghannan, Balozi wa Cuba Mhe Lucas Damingo, Balozi wa Pakistan Mhe Mohammed Salem, Balozi wa Uswis Mhe Didier Chassot, Balozi wa Ireland Mhe Mary Oneill.

Wengine ni Balozi wa Rwanda Meja Jeneral Charles Karamba, Balozi wa Syria Dr Sawsan Alani, Balozi wa Korea Mhe Kim Yong Su, Balozi wa Iran Mhe Hussein Alvandi Behined, Balozi Hispania Mhe Fransisca Pedros, Balozi wa Zambia nchini Mhe. Benson Chali na Balozi Vietnam Mhe Nguyen Namtien.

Baadhi ya Wakuu wa mashirika na Taasisi za Kimataifa waliofika kusaini kitabu cha maombolezo ni pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Mhe. Zlatan Milisic, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF, Mhe. Shahini Bahuguna,Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu,sayansi na utamaduni Mhe Tirso Do Santos,Shirika la Kazi duniani Wellingtone Chibebe,Shirika la Maendeleo la Umoja wa mataifa Mhe Christine Musisi na Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa Mhe Antonio Jose Canandula.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee  kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 jijini Dar es Salaam 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa heshima mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 jijini Dar es Salaam 


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 jijini Dar es Salaam 


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Othman Masoud akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Shinichi Goto akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Zambia nchini Tanzania, Mhe. Benson Chali akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Mary O’neill kisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Zlatan Milisic akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi. Christine Musisi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi Hispania Mhe Fransisca Pedros akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli


Balozi wa Rwanda Meja Jeneral Charles Karamba akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli