|
Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Omar Said Shabaan akifungua Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza Wawakilishi ili kuwa na uelewa wa pamoja na
kutekeleza kwa ufanisi Mkataba wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. | | | |
|
|
|
Naibu
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Exaud Kigahe akizungumza
katika Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza Wawakilishi ili
kuwa na uelewa wa pamoja na kuutekeleza kwa ufanisi Mkataba wa Eneo Huru la
Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofayika Zanzibar.
|
|
Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Omar Said Shabaan (katikati) katka meza kuu wakati wa Warsha ya pamoja ya
Wabunge na Wajumbe wa Baraza Wawakilishi kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
|
Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Biashara na Utalii katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Yussuf Hassan Iddi (katikati) akiwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt. Hashir Abdallah (kulia) Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Dkt. Aboud S. Jumbe (kushoto) wakifuatilia ufunguzi wa Warsha ya pamoja ya
Wabunge na Wajumbe wa Baraza Wawakilishi kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Washiriki wa Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza
Wawakilishi wakifuatilia ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Washiriki wa Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza
Wawakilishi wakifuatilia ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Washiriki wa Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza
Wawakilishi wakifuatilia ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Washiriki wa Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza
Wawakilishi wakifuatilia ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Baadhi ya Washiriki wa Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza
Wawakilishi katika icha ya pamoja na meza kuu baada ya ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Baadhi ya Washiriki wa Warsha ya pamoja ya Wabunge na Wajumbe wa Baraza
Wawakilishi katika icha ya pamoja na meza kuu baada ya ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
|
Wajumbe wa Sekretarieti ya AfCFTA kutoka Accra, Ghana katika picha ya pamoja na meza kuu baada ya ufunguzi wa warsha kuhusu utekelezaji wa Mkataba
wa Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) iliyofanyika Zanzibar. |
Sekretarieti ya Mkataba wa Eneo Huru la Biashara barani
Afrika (AfCFTA) limeendesha Warsha ya kujenga uelewa wa pamoja kuhusu Mkataba huo
kwa Wabunge na Wajumbe wa Baraza Wawakilishi ili kuwa na uelewa wa pamoja na
kuutekeleza kwa ufanisi.
Akifungua warsha hiyo mjini Zanzibar, Waziri wa
Biashara na Maendeleo ya Viwanda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Omar Said
Shabaan amesema uelewa wa pamoja kuhusu mkataba huo ni muhimu kwakuwa utaiwezesha nchi kuutekeleza
kwa vitendo na hivyo kunufaika na malengo ya kuanzishwa kwake.
"Kutekeleza mkataba huu lazima kuwe na uelewa
wa pamoja, hii itawezesha nchi kujipanga na kwenda pamoja kuutekeleza na hivyo kunufaisha
nchi kwa ujumla wake," alisema mhe. Omar
Amesema uelewa wa pamoja wa Mkataba huo wa AfCFTA
kutawezesha nchi kupata tija iliyokusudiwa wakati nchi ilipoamua kuuridhia na kusaini
na hivyo kuwa miongoni mwa watekelezaji wake.
Amesema Serikali zote mbilii za Muungano na ile ya
Mapinduzi Zanzibar zimeufanyia tathmini Mkataba huo na kuja na mkakati maalum
wa kusaidia utekelezaji wake
Amezitaka taasisi za uratibu wa mkataba huo
kuendeleza juhudi za kuwezesha utekelezaji wa Mkataba huo ili kufahamu na
kuzikamata fursa zinazopatikana katika soko la Mkataba huo ili kuutekeleza kwa
ufanisi na hivyo kunufaika nao.
Amesema kama nchi haina budi kuangalia fursa za
soko la AfCFTA ambalo litakuwa mbadala wa masoko mengine ambayo yana ukomo
kutegemeana na nchi inavyokua kiuchumi.
Amesema kwa ukubwa wa soko la AfCFTA unaweza
kuleta changamoto lna kueleza kuwa Serikali zimejipanga kukabiliana na changamoto
za biashara kwa kuboresha mazingira ya kufanya biashara, kuvutia wawekezaji na kuwafaanya wazalishaji
wake wawe na uwezo wa kuzalisha bidhaa zenye viwango ili kufikia mahitaji ya
bidhaa katika soko hilo la AfCFTA.
Amesisitiza kuwa utekelezaji wa Mkataba wa AfCFTA
utapelekea ukuaji wa biashara, uwekezaji na uzalishaji wa bidhaa bora kwa nchi na
hivyo kama nchi lazima itilie mkazo ili kunufaika na soko hilo.
Warsha hiyo inayoendeshwa na Sekretariati ya
AfCFTA yenye makao yake makuu mjini Accra ,Ghana ililenga kutoa elimu na
mahitaji ya Mkataba wa AfCFTA ambao Tanzania kupitia Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania iliuridhia na kuusaini mwezi Septemba 2021.
Tanzania iliwasilisha Hati ya kuuridhia Mkataba
huo kwa Kamisheni ya Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia mwezi Februari ,2022
na hivyo kuwa miongoni mwa mataifa yanayotekeleza mkataba huo.
Mkataba wa AfCFTA ulianzishwa na Wakuu wa Nchi na
Serikali za Umoja wa Afrika walipokutana katika kikao kilichofanyika jijiini Kigali, Rwanda
mwaka 2018.