|
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata
Mulamula akiwa na Waziri wa Maendeleo Ushirikiano na
Biashara ya Nje Mhe. Ville Skinnari
jijini New York walipokutana jijini humo tarehe 19 Septemba 2022. |
|
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata
Mulamula akizungumza na Waziri wa Maendeleo Ushirikiano na
Biashara ya Nje Mhe. Ville Skinnari
jijini New York walipokutana jijini humo tarehe 19 Septemba 2022. |
|
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata
Mulamula akizungumza na Waziri wa Maendeleo Ushirikiano na
Biashara ya Nje Mhe. Ville Skinnari
jijini New York walipokutana kwa mazungumzo jijini humo tarehe 19 Septemba 2022. |
|
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata
Mulamula na timu yake kulia wakizungumza na Waziri wa Maendeleo Ushirikiano na
Biashara ya Nje Mhe. Ville Skinnari
na timu yake kushoto jijini New York walipokutana jijini humo tarehe 19 Septemba 2022. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata
Mulamula (Mb) amekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Maendeleo Ushirikiano na
Biashara ya Nje Mhe. Ville Skinnari
jijini New York na kuahidi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na
Findland.
Akizungumza katika kikao hicho Balozi Mulamula ameelezea nia ya Tanzania
kushirikiana na Finland katika maeneo ya uendelezaji wa miundombinu, ICT,
Kilimo na utunzaji wa mazao ya kilimo, nishati, gesi na biashara ya hewa ukaa.
Amesema Tanzania inaliona suala la miundombinu kama ujenzi wa reli ya
kisasa (SGR) na upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam kama jambo
litakaloziunganisha nchi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini na hivyo
kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa katika kanda hizo.
Amesema suala la uwepo na upatikanaji wa uhakika wa nishati za umeme na
gesi ni miongoni mwa mambo ambayo Serikali inayatilia mkazo kwani inaamini kuwa
yakikamilika yatavutia wawekezaji wengi nchini na hivyo kukukuza uchumi wa
wananchi na taifa kwa ujumla na ndio maana serikali inawekeza nguvu kubwa
katika maeneo hayo
“Uwepo na upatikanaji wa uhakika wa nishati za umeme na gesi ni moja ya
maeneo ambayo, Serikali inayatilia mkazo na yakikamilika yatavutia wawekezaji
wengi zaidi nchini na kukukuza uchumi
wetu kwa ujumla na ndio maana serikali inaweka mkazo kukuza na kuimarisha
maeneo hayo,” amesema Balozi Mulamula
Akiongelea suala la kuimarisha sekta ya kilimo nchini Balozi Mulamula
amesema Serikali inalichukulia kwa umakini mkubwa suala hilo na ndio maana
imekuwa ikiongeza bajeti yake kila mwaka ili kuifanya sekta hiyo ikue kwa kasi
na hivyo nchi kujitosheleza kwa chakula na kuwa na ziada ya kuuza nje na
hivyo kukuza kipato chake na cha
wananchi kwa ujumla
Kuhusu eneo la ICT Balozi Mulamula amesema Serikali inatoa kipaumbele
katika eneo hilo kwa kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya mafunzo ili kuwa na
wahitimu wengi watakaokidhi mahitaji ya viwanda nchini na hivyo kuzalisha
kisasa zaidi
Naye Waziri wa Finland Mhe. Skinnari amesema Finland iko tayari
kushirikiana na Tanzania katika maeneo ya uendelezaji wa miundombinu hasa
katika mpango wa upanuzi wa bandari ya Dar es salaam na kuifanya kuwa lango
kubwa katika ukanda wa kusini na Afrika
Mashariki na kuangalia namna ya kuwa na maeneo ya kilimo bora zaidi kwa ajili
ya uzalishaji wa chakula nchini.
Ameahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo ya biashara,
uwekezaji na uendelezaji wa miundombinu ya ICT kwa kushirikiana na wadau wao
mbalimbali.
Mawaziri hao wako jijini New York kuhudhuria Mkutno wa 77 wa Baraza Kuu
la Umoja wa Mataifa (UNGA) unaoendelea nchini Marekani