Wednesday, September 21, 2022

BALOZI MULAMULA ASHIRIKI MKUTANO WA MAWAZIRI KUHUSU MAZINGIRA NA MAENDELEO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika  Mkutano wa Mawaziri kuhusu Mazingira na Maendeleo ulioandaliwa na Uingereza na Rwanda na kufanyika  jijini New York tarehe 20 Septemba, 2022 ikiwa ni mkutano wa pembezoni wakati huu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA)

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika  Mkutano wa Mawaziri kuhusu Mazingira na Maendeleo ulioandaliwa na Uingereza na Rwanda na kufanyika  jijini New York tarehe 20 Septemba, 2022

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika Mkutano wa Mawaziri kuhusu Mazingira na Maendeleo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika  Mkutano wa Mawaziri kuhusu Mazingira na Maendeleo ulioandaliwa na Uingereza na Rwanda na kufanyika  jijini New York tarehe 20 Septemba, 2022

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ameshiriki  Mkutano wa Mawaziri kuhusu Mazingira na Maendeleo ulioandaliwa na Uingereza na Rwanda na kufanyika  jijini New York tarehe 20 Septemba, 2022 ikiwa ni mkutano wa pembezoni wakati huu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) unaoendelea nchini Marekani.

Akizungumza katika mkutano huo, Balozi Mulamula amesema Tanzania imeandaa mpango maalum  utakaoongoza namna ya kukabiliana na athari za uharibifu wa mazingira kulingana na ukubwa wa athari hizo katika kila eneo nchini.

Amesema mpango huo umepangwa kulingana na ukubwa wa nchi na hali tofauti za hewa katika kila eneo, misimu ya mvua,  upepo, kiwango cha joto na shughuli za kijamii na kiuchumi katika eneo husika.

Ameongeza kuwa kupitia mpango huo changamoto 12 kuu zitokanazo na uharibifu wa mazingira ambazo ni uharibifu wa ardhi, ukataji miti, upotevu wa viumbe hai, mabadiliko ya hali ya hewa, uharibifu wa vyanzo vya maji, uharibifu wa fukwe na viumbe vya majini, usimamizi wa taka, uchafuzi wa hewa na uvamizi wa viumbe zimebainishwa na hivyo itaisaidia nchi kuchukua njia stahiki kukabiliana nayo na kuyatafutia afua zake kikamilifu

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.