Sunday, September 4, 2022

WAJUUMBE WA KAMATI YA NUU WATEMBELEA MIRADI YA KIKANDA YA EAC



Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala, Mhandisi Steven Mlote akiongea jambo wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) ilipotembelea Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mshariki jijini Arusha kabla ya kuanza kutembelea miradi ya miundombinu ya EAC inayotekelezwa mkoani humo. Mwingine katika picha ni Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vita R. Kawawa

Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akiwasilisha mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC kwa wajumbe wa Kamati ya NUU jijini Arusha.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kwa makini mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kwa makini mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota.

Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vita R. Kawawa akichangia hoja baada ya kuwasilishwa mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vicent Mbogo akichangia hoja baada ya kuwasilishwa mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Mjumbe wa Kmati ya NUU, Mhe. Janeth Masaburi akichangia jambo kuhsu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati ya NUU na wajumbe wengine wakisikiliza mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Wajumbe wa Kamati ya NUU wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Vita Kawawa wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala, Mhandisi Steven Mlote pamoja na watumishi wengine wa Serikali mbele ya Jengo la Makao Makuu ya EAC.

Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vita R. Kawawa akipokelewa na watumishi wa Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga, mara baada ya kuwasili na kamati yake katika kituo hicho kwa ajili ya kuangalia utendaji wa Kituo.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato wa Mkoa wa Arusha, Bw. Paul Kamukulu akifafanua jambo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga kwa wajumbe wa Kamati ya NUU walipotembelea kituo hicho tarehe 03 Septemba 2022.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Lungido, Bw. Kamana Juma Simba akitambulisha ujumbe wa Wilaya yake ulioshiriki katika ziara ya wajumbe wa Kamati ya NUU katika Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga

Meneja wa Mamlaka ya Mapato wa Mkoa wa Arusha, Bw. Paul Kamukulu akisoma taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga kwa wajumbe wa Kamati ya NUU
Afisa kutoka Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, Bw. Imail Abdalla akifanya majumuisho ya ziara ya Kamati ya NUU katika miradi ya miundombinu ya EAC iliyofanyika kuanzia tarehe 02 hadi 04 Septemba 2022 

Wajumbe wa Kamati ya NUU wakisikiliza majumuisho ya ziara yao kutoka kwa Afisa kutoka Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, Bw. Imail Abdalla

Mjumbe wa Kamati ya NUU, Bw. Cosato Chumi akijumuika na wajasiriamali wanaofanya biashara maeneo ya kuzunguka Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga



Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mahariki, Bw. Justin Kisoka akijumuika na wajasiriamali wanaofanya biashara maeneo ya kuzunguka Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga

Picha ya pamoja






 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.