Friday, September 2, 2022

BALOZI MULAMULA AIHAKIKISHIA JUMUIYA YA KIMATAIFA UTAYARI WA TANZANIA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akiwa katika meza kuu wakati wa hafla ya ufungaji wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam . Mkutano huo uliandaliwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania na Uingereza na kushirikisha wajumbe kutoka nchi 20 . 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam. 

 

Bw. Matt Toombs kutoka Uingereza  akizungumza katika hafla ya ufungaji wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri wa Nchi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) akimpa mkono wa pongezi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula baada ya kufunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akishukuru baada ya kufunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

 

Baadhi ya washiriki wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia hotuba ya ufungaji wa mkutano huo iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamulahayupo pichani


Baadhi ya washiriki wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia hotuba ya ufungaji wa mkutano huo iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamulahayupo pichani


 

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ameihakikishia jumuiya ya Kimataifa utayari na ushiriki thabiti wa Tanzania katika jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

 

Balozi Mulamula ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo ulioandaliwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania na Uingereza na kushirikisha wajumbe kutoka nchi 20 .

 

“Tanzania iko tayari na itaendelea kuwa mshiriki thabiti wa jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, na niwahakikishie kwamba Tanzania ni muumini wa ushirikiano wa kimataifa katika kulinda na kuhifadhi mazingira kama nguzo kanuni na miongozo ya Umoja wa Mataifa inavyosema,” alisema Balozi Mulamula.

 

 

Balozi Mulamula pia amesema Tanzania ni muumini wa ushirikiano wa kimataifa kama nguzo ya kulinda mazingira sambamba na maadili na miongozo ya Umoja wa Mataifa inavyosema.

 

Ametumia nafasi hiyo kuwasihi wajumbe wa mkutano huo na mikutano mingine kama hiyo kuhakikisha wanakuwa na ajenda moja itakayosaidia harakati za dunia katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi duniani.

 

Awali akitoa maelezo mafupi kuhusu mkutano huo Bw. Matt Toombs kutoka Uingereza alisema washiriki wa mkutano huo wamejadili maeneo mblimbali yanayohusiana na  utunzaji wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi na kukublina kuendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuona namna ya kuweza kukbiliana na changamoto hiyo.

  

Mkutano huo wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo ulioandaliwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na Serikali ya Uingereza na kushirikisha zaidi ya nchi 20 duniani ulianza tarehe 1 Septemba na kufunguliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.