Monday, August 13, 2012

WAZIRI MEMBE AZUNGUMZA NA MABALOZI WA NJE HAPA NCHINI‏

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza masuala mbalimbali na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini leo katika Ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam. Pichani ni Balozi Rajab Gamaha (kulia), Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mhe. Balozi Juma Mpango (kushoto) wa Kongo DRC ambaye pia ni Kiongozi wa Mabalozi hapa nchini. 

Baadhi ya Mabalozi, wakiwemo Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Mhe. Filiberto Ceriani Sebregondi (kulia) na Naibu Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Hans Koeppel (katikati), wakimsikiliza Mhe. Waziri Membe wakati  akizungumza nao leo katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. 
  

Baadhi ya Mabalozi, wakiwemo Balozi wa Malawi, Mhe. Flosie Asekanao Gomile-Subiaomba (wa tano kutoka kushoto) na Mabalozi kutoka nchi za Nigeria, Pakistani, Palestina, Rwanda, Somalia na nchi nyingine,  wakimsikiliza Mhe. Waziri Membe wakati akizungumza nao leo katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.