Tuesday, January 8, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

220px-Coat of arms of Tanzania.svg f1f71


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika-SADC (TROIKA) ataongoza kikao cha Wakuu wa Nchi tatu zinazounda Asasi hiyo kinachotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Alhamisi tarehe 10 Januari, 2013.

Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kitajadili maendeleo ya hali ya siasa nchini Madagascar na hali ya usalama Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Viongozi wanaotarajiwa kuhudhuria kikao hicho ni Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Troika, Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini na Rais Armando Emilio Guebuza wa Msumbiji.

Aidha, kikao hicho kitatanguliwa na kikao cha Mawaziri kitakachofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) ya jijini Dar es Salaam tarehe 09 Januari, 2013.

Nchi tatu za TROIKA ni Afrika Kusini, Namibia na Tanzania, ambaye ndiye Mwenyekiti. Nchi ya Msumbiji inashiriki kama Mwenyekiti wa sasa wa SADC.


IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM.

08 JANUARI, 2013


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.