Friday, April 5, 2013

Waziri Membe atoa msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa mpaka Ziwa Nyasa na Malawi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo tarehe 5 Aprili, 2013 kuhusu msimamo wa Tanzania wa kusubiri uamuzi utakaotolewa na Jopo la Usuluhishi linaloongozwa na Rais Mstaafu wa Msumbiji, Mhe. Joachim Chisano kuhusu mgogoro wa mpaka katika Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi.


Baadhi ya Waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya Habari wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao kuhusu msimmo wa Tanzania kuhusu mgogoro unaoendelea kati ya Tanzania na Malawi juu ya mpaka katika Ziwa Nyasa

Wanahabari wakiwa kazini.


Mhe. Membe akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani). Wengine katika picha ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (kulia) na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha.


Balozi Liberata Mulamula (kulia), Mshauri Mwandamizi wa Rais katika masuala ya Diplomasia naye alikuwepo wakati wa Mkutano wa Mhe. Membe na Waandishi wa Habari. Katikati ni Balozi Irene Kasyanju, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mhe. Shamim Nyanduga (kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji.

Mhe. Membe akiendelea kutoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu mgogoro wa mpaka katika Ziwa Nyasa unaozihusu Tanzania na Malawi huku Katibu Mkuu, Bw. Haule (katikati) na Balozi Vincent Kibwana, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakisikiliza.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.