Friday, February 21, 2014

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil  Fahmy (hayupo pichani) katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) Jijini Dar es Salaam. Mhe. Fahmy yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 21 hadi 23 Februari, 2014. Wakati wa mazungumzo hayo masuala mbalimbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususan katika nyanja za elimu, afya na uwekezaji. Kulia kwa Mhe. Membe ni Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vincent Kibwana.
Mhe. Fahmy (wa nne kutoka kushoto) kwa pamoja na ujumbe wake  wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mkutano wao.
Mhe. Membe akizungumza.
Mhe. Fahmy akieleza jambo wakati wa mazungumzo.
Mhe. Membe na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Fahmy (hayupo pichani)
Ujumbe wa Tanzania wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani)
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani).

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.