Friday, February 21, 2014

Tanzania na Misri kuimarisha ushirikiano


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Mhe. Nabil Fahmy  wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu  ziara ya siku tatu ya Mhe. Fahmy hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 23 Februari, 2014. Mhe. Fahmy yupo nchini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususan katika nyanja za afya, elimu, uwekezaji na siasa. 
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwasikiza Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani) walipozungumza nao

Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vincent Kibwana (kushoto waliokaa)  na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga wakinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Fahmy (hawapo pichani) wakati wa Mkutano wao na Waandishi wa Habari. 
Mhe. Fahmy nae akizungumza wakati wa mkutano huo.
Waandishi na Maafisa kazini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.