Friday, February 7, 2014

Mkataba kuhusu Ujenzi wa Taasisi ya kuweka kumbukumbu za kazi za iliyokuwa Mahakama ya ICTR wasainiwa.

        Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha (kulia) pamoja na Katibu Mkuu Msaidizi wa masuala ya Sheria katika Umoja wa Mataifa, Bw. Stephen Mathias (kushoto) wakisaini Mkataba kuhusu  "Suplementary Agreement to the Agreement between the United Republic of Tanzania and the United Nations concerning the Headquarters of the International Residual Mechanism for Tribunals". Taasisi hii ya Kimataifa itajengwa Jijini Arusha eneo la Lakilaki kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya kazi za iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR).

     Balozi Gamaha akibadilishana Mkataba huo na Bw. Mathias mara baada ya kuusaini

Balozi Gmaha akizungumza mara baada ya kusaini mkataba. Kulia ni Mhe. Tuvako Manongi, Balozi wa Tanzania kwenye Uwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa, New York, Marekani

Bw. Mathias kutoka Umoja wa Mataifa naye akizungumza mara baada ya kusaini Mkataba

Wajumbe waliokuwepo wakati wa kusainiwa Mkataba huo


Picha na Reginald Kisaka

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.