Friday, February 21, 2014

Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Vincent Kibwana (kushoto) akiwa na Balozi wa Misri hapa nchini, Mhe. Hossam Moharam wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakisubiri kumpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil Fahmy ambaye anatarajiwa kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 21 hadi 23 Februari, 2014.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Mhe. Nabil Fahmy (kulia) akiongozana na Mhe. Balozi Moharam mara baada ya kuwasili nchini.
Mhe. Fahmy akisalimiana na Maafisa kutoka Ubalozi wa Misri waliopo hapa nchini

Mhe. Fahmy akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili nchini.
Mhe. Fahmy akimsikiliza Balozi Kibwana wakati akifafanua jambo kwake mara baada ya kuwasili nchini
Mhe. Fahmy akizungumza na Balozi Moharam
Balozi Moharam akijadili jambo na Balozi Kibwana mara baada ya kumpokea Mhe. Fahmy.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.