Wednesday, March 18, 2015

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania awasilisha mada kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu akiwasilisha mada kuhusu  "Exchange Rate Developments in Tanzania and Implications for the Economy"  kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa Semina fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam tarehe 18 Machi, 2015.  Katika mada yake Prof. Ndulu  alielezea pamoja na mambo mengine umuhimu wa Tanzania kuuza zaidi bidhaa zake nje ili kudhibiti mfumuko wa bei na kuipandisha thamani  Sarafu ya Tanzania dhidi ya sarafu nyingine hususan Dola ya Marekani, kuimarisha upatikanaji wa fedha za nje kama dola na kuvutia zaidi wawekezaji nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (katikati) akifuatilia uwasilishwaji wa mada kutoka kwa Prof. Ndulu (hayupo pichani). Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Irene Kasyanju na kulia ni Balozi Mstaafu Elly Mtango.    
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akiwa na  Katibu wa Waziri Membe, Bw. Thobias Makoba  wakimsikiliza Prof. Ndulu ambaye hayupo nchini.
Waziri Membe akielezea jambo mara baada ya Gavana kumaliza kutoa mada 
 Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy (katikati), akiwa pamoja na Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika,  Balozi Joseph Sokoine na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano,  Bi Mindi Kasiga wakati wa Semina hiyo.
Sehemu ya Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia Semina iliyokuwa ikiendeshwa na Prof.  Ndulu.
Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia (CFR), Balozi. Omary Mohamed Maundi akiuliza swali kwa Prof. Ndulu wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam.
Prof. Ndulu akifafanua jambo
Wakurugenzi kutoka Chuo cha Diplomasia wakisikiliza semina iliyokuwa ikitolewa na Prof. Ndulu. Mwenye tai nyeusi ni Dr. Watengere Kitojo  na kulia ni Dr. Bernard Archiula.
Mchumi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Joseph Mwasota akiomba ufafanuzi wa hoja kutoka  kwa Prof. Ndulu ambaye hayupo pichani.
Prof. Ndulu akiendelea kutoa majibu yaliyokuwa yakiulizwa katika semina hiyo.
Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Paul Kabale (kushoto) akiwa na Mkaguzi Mkuu wa Ndani,  Bw. Mathias Abisai pamoja na  Mkurugenzi wa Idara ya Ununuzi, Bw. Elias Suka wakati wa semina hiyo.
Sehemu nyingine ya washiriki katika Semina hiyo
Prof. Benno Ndulu akibadilshana mawazo na Mkurugenzi wa Masomo wa Chuo cha Diplomasia Dkt. Watengere Kitojo.  
Waziri Membe akizungumza na  na Waandishi wa Habari 
Picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa Semina.

Picha na Reginald Philip na Reuben Mchome

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.