Sunday, March 29, 2015

Rais Jakaya Kikwete azindua jengo jipya lenye Ofisi za Uwakilishi wa Tanzania Umoja wa Mataifa

Rais Kikwete akikata utepe pamoja na Mhe. Mahadhi Juma Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa  na viongozi wengine, kufungua rasmi jengo la ghorofa sita la Ofisi za Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani leo Machi 29, 2015

Juu na chini ni Jengo la ghorofa sita la Ofisi za Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.  

Rais Kikwete akisaini kitabu cha wageni baada ya kufungua rasmi jengo hilo. Anayeshuhudia ni Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi 
Rais Kikwete akiandaliwa kwa picha ya pamoja na viongozi wa Wizara, Mhe. Mahadhi (aliyekaa kulia), Naibu Waziri - Nje, Balozi Tuvako Manogi, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa na Balozi Ramadhani Mwinyi (kwanza kushoto), Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa.

Baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi (Home based staff) kwenye picha ya pamoja na Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya ufunguzi wa Jengo la Tanzania.

Baadhi ya Wafanyakazi (local based staff) kwenye picha ya pamoja na Mhe. Rais Kikwete. Pia kwenye mstari wa kwanza ni Col. Mutta (wa kwanza kulia) Mwambata Jeshi wa Tanzania nchini Marekani na Canada, ambaye alihudhuria sherehe hizo NY ambapo Mwambata Jeshi wa Umoja wa Mataifa yuko masomoni. 

Viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo za ufunguzi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.