Monday, March 9, 2015

Wanawake Mambo ya Nje washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani


Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wameungana na Wanawake wengine duniani kote katika kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi mmoja, Jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alikuwa ni Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma Kikwete. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "UWEZESHAJi WANAWAKE TEKELEZA WAKATI NI SASA"


Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bibi Amisa Mwakawsago (aliyevaa miwani) akiwaongoza Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kusherehekea siku ya wanawake duaniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika maandamano.
Mama Salma Kikwete (Katikati) akiwapungia mkono wa kina Mama kutoka Wizara ya Mambo ya Nje waliokuwa wakipita mbele kwa furaha (Hawapo pichani), 
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakiwa wamejawa na furaha na bashasha kuherehekea siku ya wanawake duniani.
Wanawake  kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika Picha ya Pamoja

Picha na Reginald Philip


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.