Sunday, March 15, 2015

TASWIRA KUTOKA UMOJA WA MATAIFA JIJINI NEW YORK

 Mhe. Waziri   Simba akisalimiana na  First Lady wa Kenya Mama Margaret Kenyatta, First Lady huyu   hukimbia mbio za marathon kama njia moja wapo ya kufatua  raslimali za kuwasaidi akina mama wenzie na watoto walio katika mazingira magumu.
Mkutano huu wa mbao ni wa waki mbili unafanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika mwaka 1995 huko Beijing, China.
Pamoja na kuhudhuria mbalimbali inayohusianana Kimesheni   Kuhusu Hadhi ya Wanawake,   Mwakilishi wa Kudumu wa wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  alipata fursa ya kuwapokea na kuzungumza na wageni mbalimbali waliofika katika Uwakilishi wa Kudumu. Balozi Manongi akiwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao walikuwa  Jijini  New York  kwa shughuli za Kikazi.  
" Utanzania na uzalendo kwanza" ndivyo anavyoelekea kusema Mhe. Susan Lymo wakati yeye na wabunge wenzie   walipofika katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Mhe. Waziri Sophia Simba  akiwa na  Mbunge wa Kawe Mhe. Halima Mdee,  Katibu Mkuu Anna Maembe, na Balozi  Tuvako Manongi katika moja wa  mikutano ya pembezoni iliyokuwa  inakwenda sambamba na  majadiliano  ya jumla ya Kamisheni ya 59. Mkutano huu  uliandaliwa na  Mke wa Rais wa  Kenya Mama, Margaret Kenyata,  ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea shughuli anazozifanya  za kuwasaidia wanawake  na watoto wa nchi mwake hasa wale walio katika mazingira magumu. Kampeni yake inayoitwa Beyond Zero inalenga katika kufikisha huduma za afya


==============================================
Wajumbe wanaohudhuria Mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake, kwa wiki kuanzia jumatano hadi Ijumaa wameendelea na jukumu kubwa la kujadiliana, kuhabaridha,a kubadilishana uzoefu, kuelimisha na hata kujifunza namna ya kuzikabilia changamato mbalimbali ambazo mwanamke na mtoto wea kike wanaendelea kukabiliana nazo. 

Mkutano huu wa mbao ni wa waki mbili unafanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika mwaka 1995 huko Beijing, China. 

 Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar unaongozwa na Mhe. Sophia Simba ( Mb) Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na umekuwa ukishiriki majadiliano ya jumla na mikutano ya pembezo iliyobeba maudhui mbalimbali lakini yote yakilenga katika usawa wa jinsia na uwezeshwaji wa mwanamke.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.