Friday, March 13, 2015

Mkurugenzi wa Afrika kutoka China amaliza ziara nchini


Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara  ya Mambo ya Nje ya China, Balozi Liu Songtian akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja na  Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu ziara yake ya siku mbili aliyoifanya hapa nchini. Kushoto ni Balozi Abdulrahman Shimbo, Balozi wa Tanzania nchini China ambaye amefuatana na Mkurugenzi huyo. Kulia ni Balozi Lu Yoqing, Balozi wa China hapa nchini.
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakati wa mkutano kati yao na ujumbe wa China na Tanzania  (hawapo pichani)
Sehemu ya wajumbe wakifuatilia mkutano kati ya ujumbe wa China, Tanzania  na Waandishi wa Habari ambao hawapo pichani.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akijibu swali wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Balozi Liu nchini
Balozi Shimbo naye akizungumza wakati wa mkutano huo
Mkutano ukiendelea
 
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Balozi Liu Songtian kwa pamoja na Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Shimbo wakijadili jambo wakati wakipitia Mchoro wa Ramani ya  Bandari ya Bagamoyo namna itakavyokuwa baada ya kumalizika ujenzi wake



Balozi Liu akipata maelezo alipotembelea Kijiji cha Makumbusho cha Kaole kilichopo Bagamoyo.

Picha na Reginald Philip





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.