Friday, March 13, 2015

WAZIRI MEMBE AONGOZA MKUTANO WA MAWAZIRI WA JUMUIYA YA MADOLA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe akiongoza Mkutano wa 45 wa Kikundi Kazi cha Mawaziri wa Jumuiya ya Madola, (Commonwealth Ministerial Action Group-CMAG) unaofanyika Mjini London, Uingereza tarehe 11 na 12 Machi, 2015. Waziri Membe ni Mwenyekiti wa Kikundi Kazi hicho ambaye aliteuliwa wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola uliofanyika nchini Sri Lanka mwaka 2013. Kushoto kwa Waziri Membe ni Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Bw. Kamalesh Sharma.

 Mhe. Bernard Membe akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Bw. Sharma.
Mkutano ukiendelea




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.