Monday, March 23, 2015

Waziri Membe awaasa waimbaji wa nyimbo za injili nchini kuwa chachu ya amani na uadilifu nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard K. Membe (Mb.) amezindua albamu mbili za nyimbo za injili zinazokwenda kwa majina ya "Pisha Mbele" na "Ni Ujumbe wa Bwana" za mwimbaji Mercy Nyagwaswa katika hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika katika Ukumbi wa Ubungo Plaza uliopo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Machi, 2015. 
Askofu Mstaafu na Baba mzazi wa Mercy Askofu Nyagwaswa (wa kwanza kulia) akiwa pamoja na Mchungaji David Mangoti (wa pili kulia) na  Balozi Mstaafu Costa Mahalu wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipokuwa akihutubia wakati wa uzinduzi huo.  
Sehemu ya Wachungaji walioudhuria  uzinduzi wa albamu hiyo.
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Bi. Mercy Nyagwaswa kulia akiwa na Mwimbaji mwenzake Bi. Upendo Nkone kwa pamoja wakimsikiliza Mhe. Membe ambaye  hayupo pichani alipozindua albamu zake za "Pisha Mbele" na Ni "Ujumbe wa Bwana". Wakati wa uzinduzi huo Waziri Membe alitoa rai kwa waimbaji wa nyimbo za injili nchini kuwa chachu ya amani na uadilifu ili nchi iendelee kuwa na utulivu na upendo. 
Mhe. Membe akiendelea kuzungumza
Bi. Mercy Nyagwaswa na kikundi chake akitoa burudani kwa mgeni rasmi pamoja na wageni waalikwa katika uzinduzi wa Albamu zake
Mhe. Membe na Askofu Mtaafu Nyagwaswa pamoja na wageni waalikwa wengine wakifurahia nyimbo zilizoimbwa na Bi. Mercy wakati wa uzinduzi wa album zake. 
Waziri Membe akikata utepe kuzindua  Albamu mbili za Bi Mercy Nyagwaswa.
Waziri Membe akimpongeza Bi. Mercy kwa kuandaag Albamu mbili kwa mara moja. 
Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.