Wednesday, March 25, 2015

Rais Kikwete afungua Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Ukanda wa Kati


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano wa Wakuu wa Nchi zinazounda Ukanda wa Kati yaani Tanzania, Uganda, Burundi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Ufunguzi huo ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam ulihudhuriwa na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Burundi, Mhe. Pierre Nkurunziza na Mawaziri waliowawakilisha Marais wa DRC na Rwanda. Pamoja na mambo mengine mkutano huo ulijadili umuhimu wakuendelea kuimarisha miundombinu ya nchi za Kanda ya Kati hususan barabara, reli na bandari ili kukuza uwekezaji na maendeleo kwa ujumla.
Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Museveni nae akizungumza wakati wa mkutano huo.
Rais wa Burundi, Mhe. Pierre Nkurunziza nae akizungumza.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (kushoto) akiwa na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Samwel Sitta na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe wakifuatiliaufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Ukanda wa Kati.
Sehemu ya wageni waalikwa wakati wa ufunguzi wa mkutano huo
Marais na Mawaziri waliowawakilisha viongozi wao wakiwa katika picha ya pamoja.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.