Monday, May 25, 2015

Mkutano wa Nne wa Mabalozi kujadili mchango wa Diplomasia ya Tanzania kuelekea Dira ya Maendeleo 2025 waanza

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) na Katibu Mkuu Mteule wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi uliofanyika katika Hoteli ya Ramada, Jijini Dar es Salaam tarehe 25 Mei, 2015. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwasilisha mada kuhusu Mafanikio ya Wizara katika Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi uliofanyika katika Hoteli ya Ramada, Jijini Dar es Salaam tarehe 25 Mei, 2015. 
Mkutano ukiendelea
Sehemu ya Mabalozi wa Tanzania wakimsikiliza Mhe. Membe ambaye haonekani pichani. Kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Aziz Ponary Mlima, Balozi wa Tanzania nchini Congo, Mhe. Anthony Cheche, Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Nassor Mbarouk na Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Mhe. Chabaka Kilumanga.
Mhe. Membe akiwa na Katibu Mkuu, Balozi Mulamula pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule (wa pili kulia) na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Philip Marmo
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Peter Kalaghe akiwasilisha mada kwa niaba ya Mabalozi wa Tanzania Kanda ya Ulaya na Marekani huku Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Ali Saleh (kulia) ambaye aliwakilisha kanda ya Mashariki ya Kati, Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. John Kijazi (kushoto) aliyewakilisha kanda ya Asia na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya aliyewakilisha kanda ya Afrika wakimsikiliza.
Mabalozi wengine wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi wakifuatilia mada wakati wa mkutano wao wa nne. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi Mhe. Wilson Masilingi, akifuatiwa na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Mhe. Mugendi Zoka na Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Deodorus Kamala
Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Mhe. Daniel Ole Njoolay (wa kwanza kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. James Lugaganya (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Mashariki, Bw. Elibariki Maleko (katikati) wakifuatilia mada.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Musa Azan Zungu akizungumza wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi kuhusu jitihada zinazofanywa na kamati hiyo kuhakikisha maslahi ya Mabalozi na Watendaji wote katika Balozi za Tanzania yanalindwa ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao vizuri.
Wakuu wa Vitengo katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nao wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,   Bw. Isac kalumuna  akifuatiwa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Bw. Mathias Abisai na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi, Bw. Lucas Suka
Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Rajabu Gamaha akichangia wakati wa majadiliano ya mada mbalimbali zilizowasilishwa

Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Silima akizungumza wakati wa majadiliano kwenye mkutano wa nne wa mabalozi. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Modest Mero
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akichangia katika mjadala kuhusu kanda ya Afrika
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki akizungumza wakati wa kuchangia mada kuhusu Kanda ya Asia na Australasia. 
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Begum Taj naye akichangia hoja
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) akizungumza wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi. Pembeni yake ni Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Bi. Victoria Mwakasege
Sehemu ya Sekretarieti wakinukuu mazungumzo wakati we mkutano wanne wa Mabalozi
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Aziz Ponary Mlima akichangia mada huku Balozi Cheche na Balozi Mbarouk
Mkutano ukiendelea

Picha na Reginald Philip


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.