Saturday, May 30, 2015

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akisoma Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake Bungeni mjini Dodoma jana tarehe 29 Mei 2015.
Kutoka kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya, Mkurugenzi wa chuo cha Diplomasia, Mhe. Dkt. Mihammed Maundi wakifuatilia kwa makini hotuba ya bajeti.


Wageni waalikwa wakiwa katika ukumbi wa Bunge wakifuatilia hotuba ya bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri Membe.


Waheshimiwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani nao wakifuatilia hotuba ya bajeti.


Wageni waalikwa wakiwamo wananchi wa jimbo la Mtama la Mhe. Waziri Membe nao wakifuatilia hotuba ya bajeti ya Waziri Membe.


Kundi lingine la Waheshimiwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wakifuatilia hotuba ya bajeti.


Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Cha Diplomasia wakisikiliza Hotuba ya Bajeti liyokuwa inawasilishwa na Waziri Membe, wakiongozwa na Mwalimu wao Bwa. Jambo
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula (Wa kwanza Kushoto), Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Balozi Irene Kasyanju (katikati) na Balozi Filiberto Sebregondi wa Umoja wa Ulaya wakizungumza jambo nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje. 
Mbunge Dkt. Hamisi Kigwangala akimpongeza Waziri Membe baada ya Bunge kupitisha Bajeti wa Wizara yake
Waziri Membe akihojiwa na Paschal Mayala Mukuu wa Kampuni ya PPR
Picha na Reginald Philip






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.