Sunday, May 17, 2015

Rais wa Msumbiji awasili nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku tatu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameongozana na mgeni wake Rais wa Msumbiji, Mhe. FilipeJacinto Nyusi mara baada ya kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Rais Nyusi ameanza ziara yake ya kitaifa ya siku tatu hapa nchini kuanzia tarehe 17 hadi 19 Mei, 2015.
Rais Kikwete akiwa na Rais Nyusi kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa la Tanzania na Msumbiji zikipigwa kwa heshima ya Rais Nyusi
Mhe. Rais Nyusi akikagua Gwaride la Heshima
Gwaride la Heshima likipita mbele ya Marais
JUU na CHINI: Mhe. Rais Kikwete kwa pamoja na mgeni wake Mhe. Rais Nyusi wakifurahia burudani kutoka kwenye vikundi vya ngoma vilivyokuwepo uwanjani hapo wakati wa mapokezi. Wengine wanaoonekana kwenye picha ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe (mwenye tai nyekundu), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Mhe. Hawa Ghasia na Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. Oldemiro Baloi (mwenye miwani myeusi)
Shamrashamra za mapokezi kama inavyoonekana.




  




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.