Thursday, May 14, 2015

Waziri Membe afungua Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Bernard K. Membe (Mb) akifungua Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo. Mkutano huo ulifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Mei, 2015. Katika hotuba yake, Waziri Membe aliwahimiza Watumishi wa Wizara kufanya kazi kwa bidii na kwa kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma
 Sehemu ya Wajumbe wa Baraza  wakifuatilia hotuba ya Waziri Membe (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tisa wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Mkutano ukiendelea huku Wajumbe wa Baraza wakiwa makini kumsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Mhe. Waziri Membe akiendelea na hotuba ya ufunguzi wa baraza hilo.
  Sekretarieti ya Baraza hilo wakiendelea na kazi ya kunukuu kile kinachozungumzwa na Waziri Membe kwa kumbukumbu

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya naye akizungumza machache wakati wa Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, BibiRosemary Jairo akitoa neno la shukrani kwa Waziri Membe kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi.Mindi Kasiga ambaye pia alikuwa Mshereheshaji wakati wa mkutano huo
Waziri Membe akiwa kwenye  Picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Wawakilishi wa TUGHE Taifa na Mkoa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa Mhe.Bernard Membe (Mb) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua baraza la wafanyakazi wa wizara ya Nje na ushirikiano wa kimataifa.


Picha na Reuben Mchome


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.