Saturday, May 30, 2015

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akisoma Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake Bungeni mjini Dodoma jana tarehe 29 Mei 2015.
Kutoka kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya, Mkurugenzi wa chuo cha Diplomasia, Mhe. Dkt. Mihammed Maundi wakifuatilia kwa makini hotuba ya bajeti.
Wageni waalikwa akiwemo Mke wa Waziri Membe, Mama Dorcas Membe (wa pili kushoto) wakiwa katika ukumbi wa Bunge wakifuatilia hotuba ya bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri Membe.
Waheshimiwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani nao wakifuatilia hotuba ya bajeti.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga naye akifuatilia Hotuba ya Bajeti ilipokuwa inawasilishwa na Waziri Membe (hayupo pichani)
Mkurugenzi Mtendaji wa  Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Bw. Elishilia Kaaya na wageni wengine nao wakifuatilia Hotuba ya Bajeti ya Mambo ya Nje ilipowasilishwa Bungeni
Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa uliaoambatana na Mhe. Waziri Membe ukifuatilia hotuba ya Wizara Bungeni.
Sehemu nyingine ya Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwemo Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wakifuatilia hotuba ya bajet ya Wizara.
Wageni wa Mhe. Membe nao wakifuatilia Hotuba 
Ujumbe wa Mabalozi wanao wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakiongozwa na Mkuu wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa DRC, Mhe. Juma Alfan Mpango (kushoto) wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe
Mama Membe (wa pili kushoto) pamoja na Balozi wa Malawi hapa nchini, Mhe.Hawa Ndilowe (wa pili kulia) na wageni wengine wakisikiliza hotuba ya bajeti ya Waziri Membe
Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Cha Diplomasia wakisikiliza Hotuba ya Bajeti iliyokuwa inawasilishwa na Waziri Membe, wakiongozwa na Mwalimu wao Bw. Jambo
Mbunge Dkt. Hamisi Kigwangala akimpongeza Waziri Membe baada ya Bunge kupitisha Bajeti wa Wizara yake
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju (katikati) na Balozi Filiberto Sebregondi wa Umoja wa Ulaya wakizungumza jambo nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje. 
Waziri Membe (Wa kwanza kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Liberata Mulamula, Mbunge wa Simanjiro Mhe. Christopher Ole Sendeka na Katibu wa Waziri, Bw. Thobias Makoba wakifurahia jambo mara baada ya hotuba ya Wizara kupitishwa na Bunge 
Mbunge wa Maswa Magharibi, Mhe. John Magale Shibuda akisalimiana na Afisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Reuben Mchome katika Viwanja vya Bunge
Waziri Membe akihojiwa na Paschal Mayala Mkuu wa Kampuni ya PPR kuhusu mipango ya Wizara katika mwaka wa fedha ujao 2015/2016
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Membe (wanne kutoka kulia) akiwa katika Picha ya Pamoja na wananchi wa Jimbo la Mtama

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.