Monday, May 4, 2015

Waziri Membe afanya Mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akisalimiana naWaziri wa Mambo ya Nje wa Burundi,  Mhe. Laurent Kavakure walipokutana kwa chakula cha mchana na kufanya mazungumzo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine Viongozi hao walizungumzia masuala ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili
Waziri Membe akimweleza jambo lililomfurahisha Waziri Kavakure
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Laurent Kavakure akizungumza huku Waziri Membe akimsikiliza 
Mazungumzo yakiendelea
Waziri Kavakure akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu mteule wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Hassan Simba Yahya 
Waziri Kavakure akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa  Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Zuhura Bundala.
Mhe. Kavakure akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga
Waziri Membe (katikati) akimtambulisha Waziri wa Maliasili na Utalii (Kushoto) Mhe. Lazaro Nyalandu kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Mhe. Laurent Kavakure. 
Waziri Membe (Wa Nne kutoka Kushoto), Waziri Kavakure (wa tatu kutoka kulia), Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe. Issa Ntambuka (Wa pili kutoka kulia), Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu Mteule Balozi Simba Yahya, (wa tatu kushoto) ni Mshauri wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Balozi Hassan Lukara. 

Picha na Reginald Philip
==============================================

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA


Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz
Tovuti : www.foreign.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 


          

 20 KIVUKONI FRONT,
          P.O. BOX 9000,
   11466 DAR ES SALAAM, 
                     Tanzania.

 



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), leo amefanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Laurent Kavakure jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro. Mhe. Kavakure aliwasili nchini tarehe 03 Mei 2015.

Wakati huo huo, Mhe. Membe ataongoza ujumbe wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenda Burundi siku ya Jumatano tarehe 06 Mei 2015 kufanya mazungumzo na Serikali ya Burundi kuhusu hali ya kisiasa inayoendelea nchini humo.

-Mwisho-
Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
04 Mei 2015


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.