Wednesday, May 20, 2015

Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi lihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania



Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza na pia anakuwa Rais wa kwanza wa Msumbiji kulihutubia Bunge la Tanzania. Katika Hotuba yake nzuri Rais Nyusi iliwasifu Waasisi wa Mataifa ya Msumbiji na Tanzania na kusifia mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi hizi mbili na kuahidi kuimarisha mahusiano katika Siasa na Uchumi. Rais Nyusi alifanya ziara ya kitaifa ya siku tatu ikiwa ni ziara yake ya  kwanza tangu aingie madarakani. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) wa kwanza kushoto mstari wa pili, pamoja na Wabunge wengine wakisikiliza Hotuba kutoka kwa Mhe. Rais Nyusi (Hayupo pichani)


Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Ombeni Sefue (Kushoto) naye akisikiliza Hotuba kutoka kwa Rais Nyusi
Viongozi Mbalimbali wa Serikali wakisikiliza Hotuba ya Mhe. Rais Nyusi Bungeni. 
 Balozi wa Tanzania nchni Msumbiji, Balozi Shamimu Nyanduga (kulia)  naye akiwa bungeni akifuatilia Hotuba ya Mhe. Rais Nyusi.
Mkurugenzi wa Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge Bw. Jossey Mwakasyuka (Wa kwanza kulia), na Maafisa Mambo ya Nje (wa pili Kulia) ni Bw. Khatibu Makenga akifuatiwa na Bw. Mudrick Soraga (wa tatu Kushoto)
Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda akizungumza
Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akipokelewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda alipowasili katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma na kupata fursa ya kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (katikati) ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
Mhe. Rais Filipe Jacinto Nyusi akiwa kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa  zikipigwa.
Kikosi cha Brass Bendi cha Jeshi la Polisi kikipiga Nyimbo za Taifa mara baada ya Rais wa Msumbiji, Mhe. Nyusi kuwasili katika Viwanja vya Bungeni Mjini Dodoma
Makaribisho ya Rais wa Msumbiji, Mhe. Nyusi yakiendelea katika viwanja vya Bungeni.
Rais wa Msumbiji akikagua gwaride la Heshima wakati wa mapokezi yake mjini Dodoma.
Rais wa Msumbiji Mhe. Nyusi pamoja na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete wakiongozwa kuingia Bungeni na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda.
Rais wa Msumbiji Mhe. Nyusi na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakiongozwa na Spika wa Bunge kutoka Nje ya Bunge mara baada ya Kumaliza kulihutubia Bunge.


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika, Bi. Zuhura Bundala (wa kwanza kushoto), Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Bw. Thobias Makoba (watatu kutoka kushoto), na katikati na Bi Talha Mohamed wakiwa Bungeni. 
Rais wa Msumbiji akipokea Picha yenye mwonekano wa Jengo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Spika wa Bunge,  Mhe. Anna Makinda huku ikishuhudiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete (Wa kwanza Kulia).


Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi na Rais Kikwete wakiwa katika picha ya Pamoja na Viongozi wa Serikali na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.