Wednesday, May 13, 2015

Rais Kikwete aongoza Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC uliofanyika Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati wa  Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo uliofanyika Ikulu, Jijini Dar es Salaam kujadili hali nchini Burundi. Mkutano huo pamoja na mambo mengine ulilaani vikali jaribio la mapinduzi nchini Burundi na kuzitaka pande zote nchini humo kuhakikisha hali ya uvunjifu wa amani inakoma mara moja. 
Wajumbe wa mkutano wakimsikiliza Rais  Kikwete (hayupo pichani).
Wajumbe mbalimbali wakiwemo Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakimsiki
Wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia kwa makini hotuba ya Rais Kikwete (hayupo pichani).
Mkutano ukiendelea
Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (Watatu  kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Museveni, (aliyeshikilia kofia),  Rais wa Rwanda, Mhe. Poul Kagame, (Wa tatu kulia), Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta (wapili kulia), Naibu Rais wa Afrika Kusini, Mhe.Cyril Ramaphosa (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Bibi Nkosazana Dlamini-zuma
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Simba Yahya (aliyesimama) akijadiliana jambo na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Ladislaus Komba (Kushoto) baada ya mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC kumalizika.
Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji  Joseph Sinde Warioba (Katikati) akizungumza jambo huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bibi. Joyce Mapunjo  pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Bwa. Innocent Shiyo wakimsikiliza 

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.