Friday, May 29, 2015

Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda akutana Ujumbe wa EU hapa nchini

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Innocent Shiyo (kulia) akizungumza na Naibu Balozi wa Ujerumani hapa nchini Bw. John Reyels  ambaye pia aliongoza Ujumbe wa Jumuiya ya Ulaya (EU), kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Jumuiya hiyo pamoja na masuala mengine yanayohusu Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 29 Mei, 2015.
Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Mhe. Adam Koeler naye akichangia jambo wakati wa kikao chao na Bw. Shiyo na kulia ni Balozi wa Uholanzi hapa nchini, Mhe. Jaap Frederiks.
Wajumbe wengine walioshiriki kikao hicho akiwemo Balozi wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Malika Barak (kulia)
Bi. Upendo Mwasha (kushoto), Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo.
Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Frederiks akichangia hoja
Mkutano ukiendelea 
Bw. Shiyo akiagana na Balozi Koeler
Bw. Shiyo akifafanua jambo kwa Maafisa walioshiriki kikao kati yake na Ujumbe wa EU



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.