Friday, August 28, 2015

Balozi Mulamula, awaaga Mabalozi wa Misri na Uturuki.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, akimkabidhi zawadi Balozi wa Uturuki anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ali Dovutoglu, wakati wa hafla ya kumuaga, iliyofanyika leo 28-08-2015,katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, akimkabidhi zawadi Balozi wa Misri anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Hossam Eldine Moharam, wakati wa hafla ya kumuaga, iliyofanyika leo 28-08-2015,katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula, akizungumza katika hafla hiyo.
Balozi wa Uturuki anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ali Dovutoglu, akitoa neno la shukrani wakati wa hafla hiyo ya kumuaga, iliyofanyika leo 28-08-2015,katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Misri anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Hossam Eldine Moharam, akitoa neno la shukrani wakati wa hafla hiyo ya kumuaga, iliyofanyika leo 28-08-2015,katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Mkuu wa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, Mhe. Juma Alfan Mpango (wa pili kushoto), Balozi wa Kenya hapa nchini Mhe. Chirau Ally Makwere (wa kwanza kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) na Balozi wa Uturuki anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ali Dovutoglu wakifuatilia hafla hiyo.
Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa Nchini Mhe. Filiberto Sebregond (katikati), Balozi wa Misri anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Hossam Eldine Moharam (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika wa Wizara ya Mambo ya Nje, wakimsikiliza Balozi wa Uturuki anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ali Dovutoglu (hayupo pichani)
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi.Mindi Kasiga, akisherehesha hafla hiyo.
Waheshimiwa Mabalozi wengine wakimsikiliza Balozi wa Uturuki anayemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ali Dovutoglu (hayupo pichani)
Waheshimiwa Mabalozi mbali mbali wakimsikiliza katibu Mkuu, Balozi Mulamula (mbele katikati,aliyesimama) wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakimsikiliza Katibu Mkuu.
Baadhi ya Mabalozi na Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,wakifuatilia hafla hiyo.
Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje Redemta Tibaigana (kushoto) na Mudric Soraga,wakifuatilia hafla hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi.Mindi Kasiga (kushoto), Ofisa wa Wizara hiyo, Bi. Felista Rugambwa (katikati), pamoja na Balozi wa Burundi hapa Nchini Mhe. Issa Ntambuka, wakifuatilia hafla hiyo.
JUU NA CHINI:
Balozi Liberata Mulamula, akiwanyanyua washiriki wa hafla hiyo kwaajili ya kugonganisha glasi na kutakiana heri katika hafla hiyo.
====================

PICHA NA REUBEN MCHOME.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberarata Mulamula  amezihakikisha nchi za Uturuki na Misri kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi hizo kwa ajili ya kuletea maendeleo ya wananchi wake. Balozi Mulamula alitoa kauli hiyo katika hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwaaga Mabalozi wa nchi hizo  Mhe Ali Davutoglu na  Mhe. Hossam Moharam, waliomaliza muda wao wa uwakilishi nchini Tanzania. 

Balozi Mulamula alieleza kuwa Serikali ya Tanzania inafahari kuona matunda ya mahusiano mazuri yaliyopo na kati ya Tanzania na nchi hizo ambayo yanaendelea kukua siku hadi siku kutokana na jitihada za Balozi Davutoglu na Moharam. Baadhi ya maeneo ya ushirikiano yaliyofanikishwa na Mabalozi hao ni uratibu wa ziara za viongozi wa kitaifa baina ya nchi hizo. Aidha, alishukuru misaada mbalimbali ambayo nchi hizo imekuwa ikitoa kwa Tanzania ambayo kwa kiasi kikubwa imesaidia kuboresha maisha ya Watanzania.

Kwa upande wake, Balozi wa Uturuki, Mhe. Ali Davutoglu akiongea katika hafla hiyo alieleza kuwa Serikali ya Uturuki ilipofanya maamuzi ya kufungua Ofisi za Ubalozi Kusini mwa Bara la Afrika, Tanzania ilichaguliwa kuwa nchi ya kwanza. Alisema tokea Ubalozi huo ufunguliwe nchini Tanzania umefanikisha mambo mengi ya kimaendeleo ikiwemo kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Istanbul, Uturuki hadi Dar es Salaam na Kilimanjaro. Alisema safari hizo zimeongeza kiwango cha biashara kati ya Uturuki na Tanzania. Mhe. Balozi alisema pia kuwa nchi hiyo ipo katika mikakati ya kufungua kituo kikubwa kwa ajili ya kuwahifadhi watu wanaoishi na ulemavu wa ngozi (albinos). Kituo hicho pamoja na mambo mengine, kitakuwa na shule, hospitali na chuo cha ufundi.

Kwa upande wake, Balozi wa Misri, Mhe. Hossam Moharam alishukuru ushirikiano aliokuwa anapatiwa na watumishi wote wa Serikali ya Tanzania ambao ulimwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kipindi chake chote cha uwakilishi nchini Tanzania. Aidha alisema msingi wa uhusiano baina ya nchi hizi mbili uliwekwa na waasisi wa mataifa hayo Hayati Mwalimu NJulius Nyerere wa Tanzania na Gamal Abdel Nasser wa Misri, hivyo kazi yake wakati wa uwakilishi wake nchini ilikuwa ni kuyaendeleza mahusiano hayo. Hafla ya kuwaaga mabalazi hao ilifanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Agosti 2015.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.