Friday, August 21, 2015

Rais Kikwete amuapisha Balozi mpya wa Tanzania Nchini Zimbabwe.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akimuapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala katika hafla iliyofanyika tarehe 21-08-2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kabla ya Uteuzi huo, Luteni Jenerali Makakala, alikua Mkuu wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kunduchi Jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya viongozi waandamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Mabalozi na Maofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na familia ya Balozi Mteule Makakala wakishuhudia kiapo.
 Rais Kikwete akimkabizi Balozi Makakala nyaraka na vitendea kazi mbalimbali kama muongozo wa kazi yake mpya ya Ubalozi.
 Familia ya Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala  wakishuhudia uapisho huo.

 Mheshimiwa Balozi Makakala akisaini kiapo hicho mbele ya Mheshimiwa Rais, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, muda mfupi baada ya kula kiapo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb), Mabalozi na Maofisa kutoka Wizara hiyo, pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe.  Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, baada ya kiapo katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam Tarehe 21-08-2015.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala.
Rais Kikwete akibadilishana mawazo na Balozi Mteule Makakala (kushoto kwa Rais) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.
 Rais Kikwete akibadilishana mawazo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, muda mfupi baada ya kumuapisha kuwa Balozi.
 Rais Kikwete akibadilishana mawazo na Viongozi waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Mabalozi na Maofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, nao wakibadilishana mawazo mara baada ya hafla hiyo, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (Kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na msemaji wa Wizara Bi Mindi Kasiga wakimpongeza Balozi Mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala, mara baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam.
=========================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.