Friday, August 14, 2015

Rais Kikwete ashiriki hafla ya chakula cha jioni kuhitimisha Kongamano la Pili la Diaspora



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.
 Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Watanzania waishio Ughaibuni (Diaspora) hawapo pichani wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa ajili ya kuhitimisha Kongamano la Pili la Diaspora katika Hotel ya Serena Jijini Dar es Salaam
Mhe. Rais akisisitizia jambo kwa Watanzania waishio Nje 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Bi. Rosemary Jairo akimsikiliza Rais Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na Diaspora wakati wa hafla ya chakula cha jioni.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju (kulia) akiwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bi. Zuhura Bundala (kushoto).
Sehemu ya wageni waliohudhuria hafla hilo wakimsikiliza Mhe. Rais Kikwete (hayupo pichani).
 
Rais Kikwete akiendelea na hotuba yake
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula naye akizungumza wakati wa hafla hiyo ya chakula cha jioni.
Balozi Mulamula akiendelea kuzungumza

Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.
Wana Diaspora kutoka nchi mbalimbali na Tanzania  wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa maalum kwa ajili ya kufunga Kongamano la pili la Diaspora. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mirisho Kikwete (kushoto) akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wa NHC kwenye masuala ya Diaspora Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Bwa. Nehemia Mchechu (Kulia)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mirisho Kikwete (kushoto) akimkabidhi cheti Mkurugenzi Mtendaji kutoka Kampuni ya Huawei nchini Bw. Sung

Balozi wa China nchini, Mhe. Lu akizungumza na mdau walipo hudhuria hafla ya chakula cha jioni kwa ajili ya kuhitimisha Kongamano la Pili la Diaspora nchini 
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mugendi Zoka akibadilishana mawazo na Watanzania waishio Nje waliohudhuria hafla ya chakula cha jioni
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza  na Mkurugenzi Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju (kulia), na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bi. Zuhura Bundala

Mkurugenzi Msaidizi, Bw. James Bwana (kulia),  akibadilishana Mawazo na Afisa Mambo ya Nje Bw. Hassan Mwamweta (kushoto).
Rais Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Bi. Rosemary Jairo (kushoto) na kulia ni Mtoto wa Bi. Rosemary Jairo 
Rais Kikwete (mwenye tai nyekundu) akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na Watanzania waishio Nje.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Kamati iliyoandaa Kongamano hilo.













Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.