Wednesday, August 5, 2015

Waziri Membe amuaga rasmi Balozi wa Hispania aliyemaliza muda wa kazi nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza mbele ya Mabalazi na Wageni waalikwa wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Wizara kwa ajili ya kumuaga rasmi Balozi wa Hispania aliyemaliza muda wa kazi nchini, Mhe. Luis Manuel Cuesta Civis.  Katika hotuba yake Mhe. Membe alimshukuru Balozi Luis kwa mchango wake wa  kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Hispania. Hafla hiyo ilifanyika kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Agosti, 2015.
Balozi Luis (kulia) kwa pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaye pia ni Mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, Mhe. Juma Halfan Mpango (wa pili kulia), Balozi wa Zimbabwe na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (kushoto) wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Balozi Luis akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo pamoja na mambo mengine aliishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiririkiano wa Kimataifa na Serikali kwa ujumla kwa ushirikiano aliopata katika kipindi chote alichokuwepo nchini.
Sehemu ya Mabalozi na wagenui waalikwa wakimsikiliza Balozi Luis (hayupo pichani)
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine akizungumza machache wakati wa hafla hiyo
Mhe. Waziri Membe kwa pamoja na Mhe. Balozi Luis, Mabalozi na wageni waalikwa wakimsikiliza Balozi Sokoine ambaye haonekani pichani
Bi. Kasiga ambaye alikuwa mshereheshaji wakati wa hafla hiyo akizungumza
Balozi Luis akimweleza jambo Waziri Membe
Maafisa Mambo ya Nje walioshiriki hafla hiyo. Kushoto ni Bi. Olivia Maboko na Bi. Tunsume Mwangolombe

Mhe. Membe na Mhe. Luis wakitakiana afya njema
Mhe. Membe akimkabidhi zawadi Balozi Luis
Waziri Membe akizungumza na Balozi Luis
Waziri Membe akiagana na Balozi Luis mara baada ya hafla hiyo
Balozi Luis akiagana na Balozi Sokoin
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.