Monday, August 10, 2015

Katibu Mkuu amuaga rasmi Balozi wa Finland aliyemaliza muda wa kazi nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Libarata Mulamula akizungumza mbele ya Mabalozi na Wageni waalikwa wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Wizara kwa ajili ya kumuaga rasmi Balozi wa Finland aliyemaliza muda wa kazi nchini, Mhe. Sinikka Antila. Katika hotuba yake Balozi Mulamula alimshukuru Balozi Antila kwa mchango wake wa  kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Finland. Hafla hiyo ilifanyika kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Balozi Mulamula akiendelea kuzungumza.
Balozi Antila (Wa kwanza Kulia), Balozi wa Demokrasia ya Kongo nchini Balozi Juma Mpango (Wa pili Kutoka kulia), Balozi wa Uingereza Mhe. Dianna Melrose (Wa tatu kutoka kulia), Balozi wa Rwanda nchini Mhe. Eugene Segore Kayihura (Wa tatu kutoka kushoto), Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Egon Kochanke (Wa pili kutoka kulia) na Balozi wa Canada nchini Mhe. Alexandre Leveque wakimsikiliza Balozi Mulamula hayupo pichani 
Sehemu ya Wageni walioudhuria hafla hiyo wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani).
Balozi Antila akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo aliishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Serikali kwa ujumla kwa ushirikiano alioupata katika kipindi chote alichokuwepo nchini.
Katibu Mkuu Mhe. Balozi Mulamula (Wa kwanza kushoto) kwa pamoja na, Mkurugenzi Idara ya Amerika na Ulaya Balozi Joseph Sokoine (Wa pili kutoka kushoto), Balozi wa Umoja wa Ulaya Mhe. Filiberto Sebregond (Wa pili kutoka kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Bwa. Alvaro Rodriguez  wakimsikiliza Balozi Antila (hayupo pichani).
Balozi Antila akiendelea Kuzungumza
Balozi Mulamula na Balozi Antila wakitakiana afya njema kwa kugonganisha Glasi
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga ambaye alikuwa mshereheshaji wakati wa hafla hiyo akizungumza.
Balozi Mulamula akimkabidhi zawadi ya picha ya Mlango wa Zenji Balozi Antila.
Wageni waliohudhuria Hafla hiyo wakifurahia kwa kupiga makofi wakati Balozi Mulamula akimkabidhi Balozi Antila zawadi ya picha (Hawapo pichani).  
Balozi Mulamula (Wa pili kulia), Balozi Mpango (Wa kwanza kushoto), Balozi Antila (Wa pili kutoka kushoto), na Balozi Sokoine wakiwa katika picha ya pamoja.
Balozi Mulamula na Balozi Antila wakiwa katika Picha ya Pamoja na wageni walioudhuria hafla hiyo.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.