Friday, August 21, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi wa India na Denmark

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Denmark nchini Mhe. Einar Hebogard Jensen, Ikulu jijini Dar es Salaam leo Tarehe 21-08-2015.

Balozi mpya wa Denmark hapa nchini Mhe. Einar Hebogard Jensen, akiwasili Ikulu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Mnikulu Bw. George Bwando, anayeshuhudia (kushoto) ni Mkuu wa Itifaki Balozi Mohamed Juma Maharage.

Mhe. Einar Hebogard akipokea heshima kutoka kwa Bendi ya Jeshi la Polisi (hawapo pichani), kwa kuimbiwa nyimbo za Taifa za Denmark na Tanzania.

Mhe. Balozi Hebogard akiweka saini kitabu cha wageni Ikulu Jijini Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete.
Rais Kikwete akimpokea Balozi Hebogard baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), akisalimiana na Balozi mpya wa Denmark hapa Nchini.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine, akisalimiana na Balozi Hebogard.

Rais Kikwete akizungumza na Balozi Hebogard mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.

Picha ya Pamoja.
========
Balozi wa India

Msafara wa Balozi mpya wa India ukiingia katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam, tayari kwa kuwasilisha hati za utambulisho kwa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Balozi mpya wa India Nchini, Mhe. Sandeep Arya, akipokea heshima kutoka kwa Bendi ya Jeshi la Polisi, kwa kuimbiwa Nyimbo za Taifa za India na Tanzania.
 Mhe. Sandeep Arya, akiweka saini kitabu cha wageni Ikulu Jijini Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete.
 Rais Kikwete akipokea Hati za Utambulisho za Mheshimiwa Balozi Sandeep Arya.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), akisalimiana na Balozi mpya wa India hapa Nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki, akisalimiana na Balozi mpya wa India hapa Nchini Mhe. Sandeep Arya.
Mhe. Sandeep Arya, akiagana na Mnikulu tayari kwa kuondoka viwanja vya Ikulu, mara baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.