Friday, June 26, 2020

MKUTANO WA MAWAZIRI WA KAMATI YA SADC YA ASASI YA USHIRIKIANO WA SIASA, ULINZI NA USALAMA (TROIKA) WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM


Mkutano wa Mawaziri wa Kamati ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama kwa ngazi ya Mawaziri umefanyika kwa njia ya Mtandao (Video Conferencing) na kujadili masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama.

Mkutano huo umefanyika chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara ya Kimataifa wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Sibusiso Busi Moyo na utakutanisha Mawaziri wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mambo ya Ndani, Ulinzi pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kutoka nchi wanachama wa SADC. Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi.

Mkutano huo umehudhuriwa na nchi 16 wanachama wa SADC ambazo ni Angola, Afrika Kusini, Botswana, Comoro, DRC, Eswatini, Lesotho, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Madagascar, Namibia, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Zimbabwe na Mwenyekiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (katikati), kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nchi George Simbachawene na mwisho kushoto ni Katibu  Mkuu Wizara ya Ulinzi, Dkt. Faraji Mnyepe wakifuatilia mkutano kwa njia ya video conference, Jijini Dar es salaam

Mawaziri pamoja na baadhi ya Makatibu Wakuu/Maafisa waandamizi kutoka Tanzania wakifuatilia mkutano kwa njia ya Video Conference, jijini Dar es Salaam

Mkutano ukiendelea  





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.