Friday, June 12, 2020

KATIBU MKUU BALOZI BRIGADIA JENERALI IBUGE AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA NMB

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigadia Jenerali Wilbert A.Ibuge akiwa na Ujumbe kutoka National Microfinance Bank (NMB) punde baada ya kuwasili katika Ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma.

Ujumbe kutoka NMB ukiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Mahusiano ya Serikali,  Bi. Vicky Bishumbo ulitembelea Wizara kwa lengo la kuwasilisha mkakati wao wa namna walivyo jiandaa kuzifika fursa zinazopatikana kwenye soko la fedha la nje (kimataifa) katika kutoa huduma na kujitengenezea faida. Sambamba na hilo walionyesha namna wanavyoshiriki katika kuhudumia Wawekezaji wa nje kupitia sekta ya fedha. 

Katibu Mkuu Balozi Brigadia Jenerali Ibuge kwa upande wake amewapongeza na kuwashukuru NMB kwa namna wanavyoshirikiana na Serikali katika kujenga uchumi wa nchi na namna wanavyoshiriki katika shughuli nyingi za kuisaidia jamii, ikiwemo kutoa misaada wakati wa majanga na udhamini wao katika shughuli mbalimbali za Serikali. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigadia Jenerali Wilbert A.Ibuge akisimsikiliza Bw. Jeremiah Lymo kutoka NMB wakati akiwasilisha mada. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigadia Jenerali Wilbert A. Ibuge akichangia jambo wakati wa mazungumzo  na ujumbe kutoka NMB 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigadia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa NMB na baadhi ya Watumishi wa Wizara

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.