Thursday, June 25, 2020

NAIBU WAZIRI DKT. NDUMBARO AFANYA ZIARA KATIKA MIPAKA YA NCHI ILIYOPO MKOANI RUVUMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) anaendelea na ziara ya siku sita (6) katika maeneo ya mipaka iliyopo mkoani Ruvuma. Mpaka sasa Dkt. Ndumbaro amefanya  ziara katika mpaka wa Wenje uliopo Wilayani Tunduru, Chiwindi uliopo Wilayani Nyasa na mpaka wa Magazini uliopo Wilayani Namtumbo Mkoa wa Ruvuma. Mipaka hii inaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbuji. 


Ziara hii ambayo inatokana na utekelezaji wa majukumu  ya Wizara, ikiwemo utekelezaji wa diplomasia ya uchumi ,kujenga, kulinda na kudumisha uhusiano wa kimataifa, inalenga kuwahimiza watendaji na Mamlaka mbalimbali za Mkoa na Wilaya za Mipakani kuhusu umuhimu wa wakudumisha, kulinda, na kuendeleza uhusiano mzuri baina ya Taifa letu na nchi tunazo pakana nazo ili kustawisha biashara baina yetu na nchi tunazopakana nazo. Kadhalika, ziara hii inalenga kuhimiza umuhimu wa kulinda mipaka ya nchi na kubaini changamoto zinazowakabili wakazi wa mipakani. 

Aidha, kwa upande wake Dkt. Ndumbaro amewataka watendaji na Wakuu wa Wilaya hizo, kuendelea kuwa wabunifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, vilele kutengeneza na kuanzisha masoko ya bidhaa mbalimbali maeneo ya karibu na mipakani kwa lengo la kuchagiza biashara, ajira na kuongeza mapato ya Serikali. "Wizara tumejipanga kutekeleza mkakati wa kuhakikisha kuwa tunashiriana kwa ukaribu na wadau wanaosaidia kutekeleza majukumu ya Wizara zikiwemo Mamlaka za Mikoa na Wilaya ambazo zipo mipakani" alisema Dkt. Ndumbaro

Wakati huo huo katika ziara hii Dkt. Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na kamati za ulinzi na usalama  katika Wilaya ya Namtumbo ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Sophia Mfaume, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Julius Mtatiro na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nayasa ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Isabela Chilumba. Wakuu wa Wilaya zote tatu pamoja Wakuu vya Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Wilaya hizo kwa nyakati tofauti waliambatana na Mheshimiwa Dkt. Ndumbaro kuzuru maeneo ya Mipakani.

Wananchi wa Tunduru kwa upande wao wameishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki  kupitia Mheshimiwa Dkt. Ndumbaro, kwa kuwatembelea na kusikiliza changamoto zinazowakabili. Baadhi ya changamoto walizozitaja ni pamoja na kutokuwepo kwa huduma ya kivuko cha uhakika, barabara (kiwango cha lami) ukosefu wa huduma ya  maji safi na salama ya uhakika na umeme. Hata hivyo Dkt. Ndumbaro ameeleza  hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa na Serikali  katika kuhakikisha kuwa changamoto hizo zinatatuliwa.


Aidha, Wananchi wa Chiwindi, Wilayani Nyasa  wamemwomba Dkt. Ndumbaro kufikisha salaam na shukrani zao kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya ya kuleta maendeleo nchini, na hasa kwa kuzingatia mahitaji ya watu wa kipato cha chini. 

Dkt. Ndumbaro amezipongeza Mamlaka zilipo katika maeneo ya mipaka hiyo kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya ya kulinda mipaka, kudumisha mahusiano na nchi jirani na kwa kutekeleza kwa ufasaha dhana ya Diplomasia ya Uchumi licha ya changamoto zinazowakabili. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mhe. Sophia Mfaume, alipowasili Walayani hapo kwa lengo la kutembelea mpaka wa Magazini. Mpaka huu uliopo Wilayani humo unaiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Msumbiji.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisalimiana na Katibu Tawala Bw. Adeni Nchimbi alipowasili katika Ofisi ya Wilaya hiyo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisaini kitabu cha wageni alipowalisi Ofisi za Makao Makuu ya Wilaya ya Namtumbo.

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mhe. Sophia Mfaume akifungua Kikao kati ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb)
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisisitiza jambo alipokuwa akiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Namtumbo
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mamlaka mbalimbali wa Wilaya ya Namtumbo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akipolewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru alipowasili katika Ofisi za Makao Makuu ya Wilaya hiyo. Akiwa Wilayani Tunduru Dkt. Ndumbaro ametembelea mpaka wa Wenje unaoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Msumbiji.
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Julius Mtatiro akifungua Kikao kati ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb). 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akifafanua jambo alipokuwa akiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tunduru. Mpaka wa Wenje uliopo Wilayani humo unaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisikiliza risala kutoka kwa mwakilishi wa Wakazi wa Kijiji cha Wenje alipotembelea kijiji hicho kinachopakana na nchi jirani ya Msumbiji.  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Wenje kilichopo Wilayani Tunduru, Ruvuma.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Namtumbo. Mpaka wa Magazini uliopo Namtumbo unaiunganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akinawa mikono kufuata kanuni na taratibu za kiafya, muhimu katika kujinga na maambukizi ya COVID-19 alipotembelea mpaka wa Wenje,Wilayani Tundu kama inavyoshauriwa na Wataalam wa Afya.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mhe. Isabela Chilumba alipotembelea Wilaya hiyo. Akiwa Wilayani Nyasa  Dkt. Ndumbaro ametembelea Mpaka wa Chiwindi unaoiunganisha Tanzania na jirani ya Msumbiji. 
Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mhe. Isabela Chiluba akifungua kikao kati ya Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, Serikali ya Kijiji, Polisi wa upande wa Msumbiji na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) kilifanyika mpakani Chiwindi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akivuka Mto unaoitenganisha Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akizungumza na Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nyasa, wawakilishi wa Serikali ya Kijiji na Polisi wa upande wa Msumbiji katika kikao kilichofanyika mpaka wa Chiwindi, Nyasa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nyasa, wawakilishi wa Serikali ya Kijiji na Polisi wa upande wa Msumbiji walropo mpakani hapo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.