Thursday, November 18, 2021

BALOZI MBENNAH ATETA NA MAKAMU RAIS WA JAMHURI YA MAURITIUS

BALOZI MBENNAH ATETA NA MAKAMU RAIS WA JAMHURI YA MAURITIUS

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Mauritius mwenye makazi yake Harare, Zimbabwe, Prof. Emmanuel Mbennah amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu Rais wa Jamhuri ya Mauritius Mhe. Eddy Boissezon, GOSK.

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wameonesha kuridhishwa na ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo na kuahidi kuendelea ushirikiana katika sekta za uchumi, biashara  utalii na uwekezaji.

Makamu huyo wa Rais pia ameiipongeza Tanzania kwa ushindi wa Bw. Abdulrazak Gurnah katika Tuzo ya Amani ya Fasihi.

Oktoba 7, 2021 Mwandishi wa riwaya nchini Tanzania Abdulrazak Gurnah alitangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel kuhusu fasihi 2021.


Makamu Rais wa Jamhuri ya Mauritius Mhe. Eddy Boissezon, GOSK akiteta na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Mauritius mwenye makazi yake Harare, Zimbabwe, Prof. Emmanuel Mbennah  


Makamu Rais wa Jamhuri ya Mauritius Mhe. Eddy Boissezon, GOSK akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Mauritius mwenye makazi yake Harare, Zimbabwe, Prof. Emmanuel Mbennah  




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.