Tuesday, November 30, 2021

MKUTANO WA NANE WA MAWAZIRI WA JUKWAA LA USHIRIKIANO KATI YA CHINA NA AFRIKA WAANZA


Rais wa Senegal  na Mwenyekiti Mwenza wa mkutano wa Nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC)Mhe. Macky Sall akihutubia wakaati wa ufunguzi wa mkutano huo katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Abdou Diouf ulioko jijini Dakar.

Rais wa China na Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano wa nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) Mhe. Xi Jinping na viongozi wengine ambao walihutubia katika ufunguzi wa mkutano huo kwa njia ya mtandao.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashaariki Balozi Liberata Mulamula akifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC)jijini Dakar , Senegal.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akizungumza kitu na mmoja wa wa shiriki wa Mkutano wa nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaofanyika jijini Dakar , Senegal.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akifuatilia ufunguzi wa Mkutano wa nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaaofanyika jijini Dakar , Senegal.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akizungumza jambo na Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine (kushoto)  huku Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Dkt. Juma Malik Akil (kulia) akisikiliza baada ya ufunguzi wa Mkutano wa nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC)jijini Dakar , Senegal.

Mkutano wa Nane wha  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) umefunguliwa rasmi jijini Dakar nchini Senegal na kuhutubiwa na wenyeviti wenza kwa njia ya mtandao na moja kwa moja.

Awali mwenyekiti mwenza na Rais wa Senegal Mhe. Macky Sall alihutubia mkutano katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Abdou Diouf ulioko jijini Dakar.

Baadaye mwenyekiti mwenza ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping alihutubia mkutano huo kwa njia ya mtandao akiwa nchini China.

Mkutano huo wenye kauli mbiu ya “kuimarisha ubia wa  China na Afrika na kukuza maendeleo endelevu na kujenga jamii ya China-Afrika yenye  kesho ya pamoja katika zama mpya” unahudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya China Mhe. Wang Yi na Mawaziri wengine wa Mambo ya Nje akiwamo Balozi Liberata Mulamula .

Katika ufunguzi wa Mkutano huo ulihutubiwa pia kwa njia ya mtandao na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mhe. Felix Tshisekedi, Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Rais wa Visiwa vya Comoro Mhe. Asumani Azali, Rais wa Umoja wa Afrika Mhe. Ndiya Musa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Getterez.

Viongozi hao wote kwa umoja wao wameelezea kuridhishwa kwao na ushirikiano imara uliopo kati ya China na Afrika na kupongeza juhudi zozote zinazochukuliwa katika kuimarisha zaidi uhusiano huo.

Viongozi hao pia wameelezea juhudi mbalimbali zinazochukuliwa na nchi na viongozi wao katika harakati za kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Covid 19 ikiwa ni pamoja na kuhakikisha maelfu ya watu wa Afrika wanapatiwa chanjo kama njia mojawapo ya kukabiliana na virus hivyo.

Pia wameongelea juu ya hatua mbalimbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa na nchi husika katika kuhakikisha mabadiliko ya hali ya hewa hayaleti changamoto zaidi kwa nchi zao.

 Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamesisitiza juu ya umuhimu wa kuendelea kuzingatia uimarishaji na ukuzaji wa demokrasia, haki za binadamu, usawa wa kijinsia na utawala wa sheria katika nchi zao

Katika hotuba yake rais wa China aliahidi kutoa dozi bilioni moja za chanjo ya covid 19 kwa nchi za Afrika ikiwa ni ziada ya dozi ambazo zimeshatolewa na China kwa nchi hizo.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.