Tuesday, November 2, 2021

MKUTANO WA 32 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA KISEKTA LINALOSHUGHULIKIA MASUALA YA AFRIKA MASHARIKI NA MIPANGO WAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA

Mkurugenzi Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi (kati) akiongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa maandalizi ngazi ya wataalamu unaofanyika jijini Arusha, Tanzania tarehe 1 na 2 Novemba 2021.

Mkutano huo wa ngazi ya wataalamu na mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 3 na 4 Novemba 2021 ni sehemu ya mikutano ya maandalizi kuelekea Mkutano wa 32 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango utakaofanyika tarehe 5 Novemba 2021. 

Wataalamu wengine waandamizi walioambatana na Balozi Mbundi ni pamoja na Mkurugenzi wa Uendeshaji Sera Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Agnes Meena (kushoto) na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka.

Mwenyekiti wa Mkutano ngazi ya wataalamu Dkt. Alice Yalla kutoka Kenya akiongoza mkutano huo unaofanyika jijini Arusha, Tanzania tarehe 1 na 2 Novemba 2021.

Ujumbe wa Uganda ukifuatilia mkutano.

Ujumbe wa Burundi ukifuatilia mkutano

 

Ujumbe wa Kenya ukifuatilia mkutano

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.