Monday, November 15, 2021

WAZIRI MULAMULA AAGANA NA BALOZI WA KOREA KUSINI

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Tae-ick Cho wakati alipokwenda kumuaga Mhe. Waziri katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimueleza jambo Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Tae-ick Cho katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Tae-ick Cho akimkabidhi zawadi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula alipofika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam kumuaga
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi ya picha ya jahazi Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Tae-ick Cho katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Tae-ick Cho katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Caesar Waitara.

 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kumuaga Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini Mhe. Tae-ick Cho katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

  “Katika kipindi chake cha uwakilishi ameiwakilisha vyema nchi yake na kufurahishwa na namna ushirikiano baina ya Tanzania na Korea ya Kusini ulivyoimarika hasa katika miradi ya maendeleo ya kimkakati na nimemuomba aendelee kuwa Balozi mzuri wa Tanzania huko aendako,” amesema Balozi Mulamula.


Nae Balozi wa Korea ya Kusini aliyemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini, Mhe. Tae-ick Cho ameipongeza Tanzania kwa hatau mbalimbali za maendeleo ya kiuchumi, kijamii  na kisiasa ambazo imekuwa ikizichukua chini ya Uongozi imara wa Rais Samia Suluhu Hassan.

 

 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.