Wednesday, November 3, 2021

BALOZI FATMA AFUNGA MKUTANO WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU

 

Balozi Fatma Rajab akizungumza katika hafla ya kufunga Mkutano wa Kimataifa wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam

 

Balozi Fatma Rajab (kushoto) akizungumza katika hafla ya kufunga Mkutano wa Kimataifa wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wanasheria waandamizi kutoka katika nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kulia  kwake ni Rais wa Mahakama hiyo Mhe. Jaji Iman Abood kutoka Tanzania.

Balozi Fatma Rajab (kushoto) akizungumza katika hafla ya kufunga Mkutano wa Kimataifa wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam

Balozi Fatma Rajab (katikati) akiwa meza kuu wakati wa hafla ya kufunga Mkutano wa Kimataifa wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam

 

Washiriki wa Mkutano wa Kimataifa wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia hafla ya ufungaji wa mkutano huo

Washiriki wa Mkutano wa Kimataifa wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia hafla ya ufungaji wa mkutano huo. 

 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Fatma Rajab amefunga Mkutano wa siku tatu wa Kimataifa wa Utekelezaji wa maamuzi ya  Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo pia uliangalia changamoto ambazo nchi wanachama wa Umoja wa Afrika unakabiliana nazo katika kutekeleza maamuzi yanayotolewa na Mahakama hiyo na kuzitafutia njia ya kukabiliana nazo pamoja na matarajio ya kuanzishwa kwa Mahakama hiyo.

Akizungumza wakati wa kufunga Mkutano huo Balozi Fatma amewataka washiriki wa mkutano huo kuyachukua yale yote waliyokubaliana katika mkutano huo ili kuziwezesha nchi zao kutekeleza maamuzi yanayotolewa na Mahakama hiyo kwa ufanisi.

Mkutano huo ulianza Novemba  Mosi umehudhuriwa na Wanasheria waandamizi kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.