Thursday, November 4, 2021

MKUTANO WA MAKATIBU WAKUU WANAOSHUGHULIKIA MASUALA YA AFRIKA MASHARIKI NA MIPANGO KATIKA NCHI ZA EAC UNAFANYIKA JIJINI ARUSHA

Mkutano wa Makatibu Wakuu wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanyika jijini Arusha, Tanzania tarehe 4 Novemba 2021.

Mkutano huu na mkutano wa ngazi ya wataalamu uliofanyika tarehe 1 na 2 Novemba 2021 ni sehemu ya mikutano ya awali kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa 32 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango utakaofanyika jijini Arusha tarehe 5 Novemba 2021.

Mikutano hii ya awali pamoja na mambo mengine ina jukumu la kupitia na kuwasilisha agenda na mapendekezo ya masuala mengine ya kikanda yatakayojadiliwa katika mkutano wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Makatibu Wakuu unaongozwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro ambaye amemuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine.

Viongozi wengine walioambatana na Dkt. Ndumbaro katika mkutano huo ni pamoja na; Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Evaristo Longopa, Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda – Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Harshil Adballah, na Afisa Mtendaji Mkuu, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) Bw. Nicodemus Mkama.


Mwenyekiti wa Mkutano wa Makatibu Wakuu ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Kenya, Mhe. Dkt. Kevit Desai (wa pili kushoto) akiongoza Mkutano wa Makatibu Wakuu unaofanyika jijini Arusha tarehe 4 Novemba 2021 kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa 32 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango utakaofanyika jijini Arusha tarehe 5 Novemba 2021.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro (kulia) akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Makatibu Wakuu wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango katika Nchi za Afrika Mashariki, Kushoto ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Evaristo Longopa.

Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda – Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Harshil Adballah, na Afisa Mtendaji Mkuu, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) Bw. Nicodemus Mkama wakifuatilia mkutano.

Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi na Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Sera Ofisi ya Rais, Menejementi ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi Agnes Meena wakifuatilia mkutano.

Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka na Afisa Biashara Mkuu katika Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Abdul Chacha wakifuatilia mkutano. 

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mkutano.

Ujumbe wa Burundi

Ujumbe wa Kenya

Ujumbe wa Uganda

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.